HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, December 4, 2021

Rais Samia aweka jiwe la msingi Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka awamu ya pili (BRT II) Dar

 KATIKA Kuelekea Miaka 60 ya Uhuru- Mhe. Rais Samia aweka jiwe la msingi Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka awamu ya pili (BRT II) katika Barabara ya Kilwa -Chang’ombe-Sokoine na Kawawa

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisogeza kitambaa kuashiria uwekaji wa jiwe la Msingi Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka Awamu ya pili (BRT II) katika Barabara ya Kilwa-Chang’ombe-Sokoine na Kawawa katika sherehe zilizofanyika Mbagala Mkoani Dar es Salaam leo tarehe 04 Desemba, 2021. Wa kwanza kulia ni Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa, Wengine katika picha ni Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Mbagala hawaonekani pichani mara baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka Awamu ya pili (BRT II) katika Barabara ya Kilwa-Chang’ombe-Sokoine na Kawawa zilizofanyika Mbagala mkoani Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

Moja ya Kituo Kikubwa cha Mabasi yaendayo Haraka Awamu ya pili (BRT II) kilichopo Mbagala mkoani Dar es Salaam.
Sehemu ya Wananchi waliohudhuria sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka Awamu ya pili (BRT II) katika Barabara ya Kilwa-Chang’ombe-Sokoine na Kawawa zilizofanyika Mbagala mkoani Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa TANROADS Eng. Rogatus Mativila wakati akitoa maelezo ya Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka Awamu ya pili (BRT II) katika Barabara ya Kilwa-Chang’ombe-Sokoine na Kawawa kabla ya kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Mradi huo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipiga makofi pamoja na viongozi Wengine mara baada ya kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka Awamu ya pili (BRT II) katika Barabara ya Kilwa-Chang’ombe-Sokoine na Kawawa katika sherehe zilizofanyika Mbagala Mkoani Dar es Salaam leo tarehe 04 Desemba, 2021.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad