NA
KHALFAN SAID, K-VIS BLOG, MBEYA
WAZIRI
wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye
Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama ameupongeza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF)
kwa kuipatia vitendea kazi (computers) Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) ili
kuharakisha shughuli za usuluhishi wa migogoro ya kikazi.
Pongezi
hizo zimetolewa na Mhe. Waziri wakati akikabidhi computer 10 kwa Mkurugenzi
Mkuu wa CMA, Bw.Shanes Nungu katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF)
jijini Mbeya Novemba 29, 2021.
“Tunashuhudia
hapa Workers Compensation Fund (Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi) unafanya kazi nzuri ya kuiwezesha CMA ili itekeleze majukumu yake sawasawa jambo
hili lina tija katika utendaji.” Alifafanua Mhe. Waziri.
Kipekee
napenda kuwashukuru sana sana wakuu wote na viongozi wa taasisi zote Dkt. John
Mduma Mkurugenzi Mkuu wa WCF na ndugu Shanes Nungu Mkurugenzi Mkuu wa CMA kwa
kuona umuhimu wa kufanya kazi kama serikali moja, ninyi wote mko chini ya
umbrella (mwamvuli) mmoja, hakikisheni kwamba mmoja anapogundua changamoto
ya mwenzake anaamua kusimama pamoja naye na kumsaidia, Alisisitiza Mhe. Waziri
Jenista Mhagama
Mhe. Waziri Jenista alisema Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umekuwa ukifanya
vizuri katika utekelezaji wa majukumu yake tangu uanzishwe miaka sita iliyopita. "Kwa sheria iliyokuwepo kabla ya kupata uhuru, ilikuwa mfanyakazi akiumia analipwa fidia ya shilingi 108,000/= bila kujali amepata ulemavu wa aina gani, kwani malipo ya fidia yalikuwa kwenye flat rate". Alieleza.
Serikali iliamua kuboresha fidia kwa Wafanyakazi kwa kuanzisha mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) amba umechukua jukumu la kulipa fidia stahiki kwa mfanyakazi atakayepatwa na madhara wakati kutokana na kazi. Alibainisha
Alisema
katika muktadha huo huo wa kugawa majukumu kiutendaji Serikali ilianzisha CMA ili ishughulike na masuala ya usuluhishi
na uamuzi inapotokea migogoro kazini.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. John Mduma alisema, makabidhiano hayo ya ni utekelezaji wa maagizo kwani ambapo kwa kufanya kazi kwa ushirikiano ndipo tunaweza kufikia malengo yetu kama Taasisi lakini pia kwa pamoja chini Ofisi moja.
“Kwa
kufanya kazi kwa pamoja ndipo tunaweza kufikia malengo yetu kama taasisi lakini
kwa pamoja kama ofisi yako Mheshimiwa Waziri, tunatambua kwamba mmoja wetu kama
atakimbia mbio na uwezo wake alionao na akawaacha ndugu zake nyuma “hatatoboa
yeye peke yake”. Alisema Dkt. Mduma.
Naye
Mkurugenzi Mkuu wa CMA, Bw. Shanes Nungu alimshukuru Waziri Jenista kwa maono
yake na kuwezesha CMA kupata msada huo wa computer ambapo hii ni mara ya pili kupata msada kutoka WCF.
“Mheshimiwa
Waziri maagizo yako yamemezaa matunda na sasa msada huu utakwenda kuongeza nguvu kwenye ule wa awali tulioupata mwanzo kutoka WCF ambao ulisaidia kutatua malalamiko ya
wananchi na ucheleweshaji wa hukumu zao umepungua.” Alishukuru Bw. Nungu.
Hafla
hiyo ilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu,
Bunge) Bw. Kaspar Muya, wakurugenzi wa WCF na CMA pamoja na watumishi wa taasisi
zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu ambazo ni NSSF, PSSSF, OSHA na Idara ya
Kazi.
No comments:
Post a Comment