HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 22, 2021

RAIS WA ZANZIBAR ALHAJ DKT. HUSSEIN ALI MWINYI AJUMUIKA NA WANANCHI KATIKA MAZIKO YA BABA MZAZI WA MJANE WA MAALIM SEIF

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ikisomwa na Katibu wa Mufti. Sheikh.Khalid Ali Mfaume, na (kulia kwa Rais) Mtoto wa Marehemu na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, wakiitikia dua baada ya kumalizika kwa Sala ya Jeneza kuusalia mwili wa Baba Mzazi wa Mjane wa Maalim Seif Sharif Hamad, Mama Awena Sanani Masoud,iliofanyika katika Msikiti wa Masingini Wilaya ya Magharibi “A” Unguja leo 22-11-2021, na (kushoto kwa Rais) Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Saleh Omar Kabi.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwafariji Watoto wa Marehemu Sanani Masoud, baada ya kumalizika kwa Sala ya Jeneza iliofanyika katika Msikiti wa Masingini Wilaya ya Magharibi “A” Unguja leo 22-11-2021.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kutowa mkono wa pole kwa Mjane wa Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad.Mama Awena Sanani na familia yake, alipofika nyumbani kwa marehemu masingini Wilaya ya Magharibi”A” Unguja kutowa mkono wa pole kwa familia leo 22-11-2021.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiitikia dua ya kumuombea Baba Mzazi wa Mjane wa Maalim Seif Sharif Hamad Mama Awena Sanani Masoud, alipofika nyumbani kwa marehemu kutowa mkono wa pole kwa Familia ya Marehemu leo 22-11-2021.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad