Mkuu
wa wilaya Ilala, Mheshimiwa Ng’wilabuzu Ndwata Ludigija, amewapongeza
vijana wanaochangamkia fursa za kiuchumi ikiwamo bahati nasibu ya Biko,
akisema wanaisaidia serikali kukuza pato lao badala ya kusubiri
kuwezeshwa tu na kuendeleza umasikini kwa wananchi.
Mheshimiwa
Ludigija ameyasema hayo wakati anamkabidhi sh milioni 10 Eugine Paullo
Mbassa alizoshinda katika droo kubwa ya bahati nasibu ya Biko
inayoongoza kutoa washindi wengi wakiwamo wa papo kwa hapo kuanzia sh
2500 hadi milioni 5 bila kusahau zaidi ya sh milioni 40 kila Jumapili.
“Nawapongeza
vijana mnaochangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwamo kucheza Biko
kwakuwa zinapunguza ukali wa maisha kwasababu isingekuwa Biko kwako
wewe ina maana ingebidi uwezeshwe na mikopo ya vijana Halmashauri,
lakini sasa serikali itaendelea na wengine kwakuwa wewe umeshafanikiwa
kwa kupitia Biko,” Alisema dc Ludigija huku akimtaka Mbassa kuzitumia
vizuri fedha za Biko.
Biko imaweza kuchezwa live kwa kuingia www.biko.co.tz pamoja
na wanaotumia simu za kawaida kwa kuweka namba ya Kampuni ya 505050 na
kumbukumbu 2456 huku kianzio cha kucheza kikiwa ni sh 1000 na kuendelea.
Wakati
washindi wa Biko papo kwa hapo wakipatikana kila baada ya sekunde moja
kwa kuchungulia nafasi kwenye gurudumua mchezo huo, wanaoshinda droo
kubwa wanakabidhiwa fedha zao bank sanjali na kuwaelekeza namna bora ya
kuzitumia fedha zao kwa kukuza pato lao.
Mheshimiwa
Mkuu wa wilaya Ilala Ng'wilabuzu Ndwata Ludigija mwenye suti akiwa
katika makabidhiano ya sh milioni 10 za Biko kwa mshindi wake Eugine
Paullo Mbassa katikati. Mwingine kulia ni Meneja Masoko wa Biko Goodhope
Heaven na kushoto ni balozi wa Biko Kajala Masanja.
Mkuu
wa Wilaya Ilala Mheshimiwa Ng’wilabuzu Ndwata Ludigija kulia akiwa na
mshindi wa sh milioni 10 kutoka bahati nasibu ya Biko Eugine Paullo
Mbassa katikati wakati wa makabidhiano ya fedha hizo katika tawi la bank
ya NBC Viwandani jijini Dar es Salaam. Kushoto kwa mshindi ni Kajala
Masanja Balozi wa Biko. Picha na Mpigapicha wetu.
Mheshimiwa
Mkuu wa wilaya Ilala Ng’wilabuzu Ndwata Ludigija mwenye suti akiwa
katika makabidhiano ya sh milioni 10 za Biko kwa mshindi wake Eugine
Paullo Mbassa katikati. Mwingine kulia ni Meneja Masoko wa Biko Goodhope
Heaven na kushoto ni balozi wa Biko Kajala Masanja.
No comments:
Post a Comment