HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, October 23, 2021

WADAU WA MAENDELEO, MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI WAKUTANA DODOMA KATIKA WIKI YA AZAKI

  


Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Francis Kiwanga (katikati) akiwa na wadau wa Maendeleo Balozi wa Canada Nchini Tanzania Hellen Fytche (kulia.)

Na Said Mwishehe,Michuzi TV - Dodoma

NI Wiki ya AZAKI! Hivyo ndivyo unavyowezea kuelezea wiki hiyo ambayo imeanza leo Oktoba 23 hadi Oktoba 28 mwaka huu Mjini Dodoma ambapo viongozi kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za umma na binafsi wamekutana kujadili na kuweka mikakati ya namna Bora kuhakikisha AZAKI zinashiriki kikamilifu kuchagiza uchumi wa Taifa la Tanzania.

Katika Wiki ya AZAKI inayokwenda na kauli mbiu inayosema AZAKI na Maendeleo imeanza mapema leo kwa wadau mbalimbali kushiriki matembezi yaliyoanzia Shule ya Sekondari Dodoma na kumalizikia  viwanja vya Ukumbi wa Jakaya Kikwete.

Wadau hao kutoka kwenye AZAKI baadhi yao walikuwa wamebeba mabango yenye jumbe mbalimbali na mengi kati yao yalikuwa yakielezea namna mashirika yasiyokuwa ya kiserikali ambavyo yamejipanga kushiriki Katika kuleta maendeleo ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan aliyedhamiria kuboresha hali ya uchumi wa watanzania.

Kwa kukumbusha tu Wiki ya AZAKI ni jukwaa pekee nchini linaloleta kwa pamoja wadau wakuu wa maendeleo ikiwemo serikali, sekta binafsi na Asasi za kiraia pamoja na wananchi kwa lengo la kujadili masuala yanayohusu ustawi wa nchi na Maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Wakati wa matembezi hayo baadhi ya washiriki wameiambia Michuzi TV na Michuzi Blog kwamba wameshiriki kwenye Wiki ya AZAKI mwaka huu kwa kutambua mchango wao Katika kuleta maendeleo kwa kutoa elimu inayowesesha kufahamu shughuli wanazofanya ambazo kimsingi ni kusaidia kupaza sauti na kuibua changamoto zikitatuliwa nchi inaendelea kupiga hatua.


Wadau mbalimbali wakiwa katika matembezi ya Wiki ya Azaki iliyoanza leo Oktoba 23 na kuendelea hadi Oktoba 28 mwaka huu wakiingia viwanja vya ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma yakitokea sekondari ya Dodoma.


Washiriki wa matembezi ya Wiki ya AZAKI wakiwa wameshika mabango yenye jumbe mbalimbali zinazohusu Asasi za Kiraia ikiwa ni siku ya kwanza ya Wiki ya Asasi za Kiraia iliyozinduliwa leo Jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Francis Kiwanga (katikati) akiwa na wadau wa Maendeleo Balozi wa Canada Nchini Tanzania Hellen Fytche (kulia.)

Meneja Miradi wa FCS Francis Uhadi (katikati) akia na Ms Rachel Chagoja (kushoto) Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la HakiRasilimali - Mtandao wa Asasi za Kiraia unaofanyakazi za kimkakati katika Sekta ya Madini, Mafuta na Gesi, wakiwa wameshika Bango lenye ujumbe usemao (Azaki zinachangia kuboresha Afya) wakati wa matembezi hayo Jijini Dodoma.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad