Mamlaka
ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam inatekeleza mradi wa
kupeleka maji maeneo ya Mbezi Mshikamano katika Manispaa ya Ubungo mkoa
wa Dar es Salaam ikiwa ni muendelezo wa jitihada wa zake za kuboresha
huduma katika maeneo mbalimbali yenye changamoto ya upatikanaji wa maji.
Mradi huu utakapokamilika utakamilisha asilimia 100 za upatikanaji wa
majisafi mkoa wa Dar es Salaam.
Akizungumza
wakati wa utiaji wa saini ya utekelezaji wa mradi wa maji Mshikamano
amesema Serikali itatoa pesa kwa ajili yabutekezaji wa mradi huo ili
kuweza kuiongezea DAWASA nguvu ya kumaliza shida ya maji katika Jimbo la
Kibamba ikiwemo mradi wa maji Mshikamano uliosainiwa leo.
Pia
ameitaka DAWASA kusimamia miradi ya maji ili kuepuka kuhujumiwa na
wananchi wasiokuwa na nia nzuri ya utakelezaji wa miradi ili kumalizika
kwa wakati na kuutaka uongozi wa Wilaya ya Ubungo kuwa wakali kwenye
mradi huo.
Aweso
amewata DAWASA kutowabambikizia wateja wa maji bili ambazo zinakuwa
kikwazo kwa wananchi na hivyo amewataka wateja wa maji kusoma Mita za
maji wakiwa na wafanyakazi wa DAWASA.
Akizungumza
wakati wa kuingia mkataba na Mkandarasi Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA
Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema utekelezaji wa wa mradi huo unahusisha
ulazaji wa Bomba la chuma lenye ukubwa wa kipenyo cha inchi 16 ambalo
litakuwa na unbali wa Kilometa 0.35 kutoka kwenye Bomba kuu la inchi 30
linalosafirisha maji kutoka Mtambo wa Ruvu Juu hadi kwenye Kituo cha
kusukumia maji eneo la Mbezi Inn.
Pia
amesema katika mradi huo kutajengwa Kituo cha kupokea na kusafirisha
maji ambacho ndani yake kutakuwa na tenki la kupokea maji litakalokuwa
na ujazo wa Lita 540,000 pamoja na jengo la pampu ikiwemo ununuzi na
ufungaji wa pampu.
"Mradi
huu utakuwa na uwezo wa kusafirisha kiasi cha Lita Milioni 23,300 za
maji kwa siku ambazo zitatosheleza mahitaji ya wananchi 179,476 ambayo
ni mahitaji ya miaka 20 ijayo." alisema Mhandisi Luhemeja
Maeneo
yatakayonufaika na mradi huo ni Mshikamano, Mpiji, Magohe, Msakuzi
Kusini, Msakuzi Kaskazini, Machimbo, Majengo Mapya, Dodoma, Luguruni
Lapaz, Mbezi Inn, Magari Saba, Magayana, Njia Panda Makondeni, TAKUKURU,
Kwa Gamba, Luguruni Dampo, Luguruni KKKT, Rising Star, Msakuzi
Supermarket, Aman Street, Miti Mirefu, Madafu, Kwa Mfala, Chikongowe,
Masaki Street, Mbezi Msumi, Machimbo na Mageti.
Mradi huu utakanilika kwa muda wa miezi 12 na unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba 15, 2021 na kukamilika Oktoba 2022.
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso akishuhudia utiaji saini wa mradi wa maji
Mshikamano kati ya Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi
wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja(kulia)
pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Advert Construction ltd Dhriv
Jog(kushoto) uliofanyika leo katika eneo la Msakuzi Center wilaya ya
Ubungo Mkoani Dar es Salaam.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja(kulia) pamoja na Mkurugenzi
Mtendaji wa Advert Construction Ltd Dhriv Jog(kushoto) wakibadirishana
mkataba wa utekelezaji wa wa mradi wa maji Mshikamano ukiofanyika katika
eneo la Msakuzi Center wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es Salaam leo
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja(kulia) pamoja na Mkurugenzi
Mtendaji wa Advert Construction ltd Dhriv Jog(kushoto) wakionesha
mkataba wa utekelezaji wa wa mradi wa maji Mshikamano ukiofanyika katika
eneo la Msakuzi Center wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es Salaam leo
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akitolea maelezo kwa Waziri wa
Maji Jumaa Aweso, Mkuu wa wilaya ya Ubungo Kheri James na Mbunge wa
Jimbo la Kibamba Issa Mtemvu kuhusu utakelezaji wa mradi wa maji
Mshikamano wakati wa hafla ya utiaji saini wa mradi huo uliofanyika leo
Ubungo Mkoani Dar es Salaam.
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso akizungumza na uongozi wa DAWASA pamoja na
wananchi wa Jimbo la Kibamba kuhusu namna Serikali ilivyojipanga
kuisimamia miradi ya maji ili kuweza kuondoa kero za upatikanaji wa maji
kwa wananchi ili kumtua mama ndoo kichwani wakati wa hafla iliyofanyika
katika eneo la Msakuzi Center wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es Salaam
leo.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es
Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza kuhusu utakelezaji
wa mradi wa maji Mshikamano pamoja na kutoa ufafanuzi changamoto
mbalimbali zinazotokea katika majimbo 16 yanayohudumiwa na na Malmala ya
Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) pamoja na
kufikisha maji katika maeneo ya Vikindu.
Kaimu
Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam
Kate Kamba akitoa salamu za Bodi wakati wa utiliwaji saini za
utekelezaji wa mradi wa Maji Mshikamano katika hafla iliyofanyika katika
eneo la Msakuzi Center wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es Salaam.
Mkuu
wa wilaya ya Ubungo Kheri James akizungumza kuhusu wananchi kulinda
miradi wakati na baada ya kumalizika kwa miradi hiyo wakati wa utiaji
saini wa mradi wa utekelezaji wa mradi wa maji Mshikamano ukiofanyika
katika eneo la Msakuzi Center wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es Salaam.
Mbunge
wa Jimbo la Kibamba Issa Mtemvu akizungumza kuhusu namna wananchi wa
Jimbo la Kibamba walivyopata changamoto za maji kwa zaidi ya miaka 10
na kutoa shukrani kwa DAWASA kwa kuweza kutekeleza miradi mbalimbali ya
maji hasa kumletea mameneja wambao anasaidiana nao ili kuweza kutekeleza
upatikanaji wa maji katika Jimbo hilo.
Waziri
wa Maji, Jumaa Aweso akipikea maji kutoka mmoja wa wananchi waliofika
kwenye hafla utiaji saini Wa mradi wa maji Mshikamano uliyofanyika
katika eneo la Msakuzi Center wilaya ya Ubungo Mkoani Dar es Salaam leo.
Baadhi
ya Wakurugenzi wa DAWASA, Meneja wa DAWASA, wafanyakazi wa DAWASA
pamoja na wananchi wa wilaya ya Ubungo wakifuatilia utiaji saini mradi
wa maji Mshikamano ukiofanyika katika eneo la Msakuzi Center wilaya ya
Ubungo Mkoani Dar es Salaam leo
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wakurugenzi wa DAWASA mara baada ya
kumalizika kwa hafla ya utiaji saini wa mradi wa maji Mshikamano
uliyofanyika leo
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja wa mikoa ya DAWASA mara baada ya
kumalizika kwa hafla ya utiaji saini wa mradi wa maji Mshikamano
uliyofanyika leo
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na madiwani wa Manispaa ya Ubungo mara
baada ya kumalizika kwa hafla ya utiaji saini wa mradi wa maji
Mshikamano uliyofanyika leo
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa Mkandarasi wa mradi Advert
Construction Ltd mara baada ya kumalizika kwa hafla ya utiaji saini wa
mradi wa maji Mshikamano uliyofanyika leo.
Waziri
wa Maji Jumaa Aweso, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majisafi na
Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Cyprian Luhemeja
wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Ulinzi na Usalama wa wilaya
ya Ubungo mara baada ya kumalizika kwa hafla ya utiaji saini wa mradi
wa maji Mshikamano uliyofanyika leo
No comments:
Post a Comment