WAZIRI
 MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na 
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imedhamiria kutekeleza dhana ya 
uchumi jumuishi kwa vitendo kwa kuweka vipaumbele vitakavyowawezesha 
wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.
Ameyasema
 hayo leo (Jumatatu, Oktoba 4, 2021) wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 
Tano la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, jijini Dodoma. Amesema kuwa 
vipaumbele katika mipango ya Serikali vimekuwa katika utekelezaji wa 
shughuli za kiuchumi zinazowajumuisha moja kwa moja wananchi.
Waziri
 Mkuu ametaja baadhi ya vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja na uimarishaji 
wa huduma za afya, hifadhi ya jamii, maji, umeme na utekelezaji wa 
mpango wa elimumsingi bila ada “Mtanzania mwenye afya, aliyeelimika na 
miundombinu wezeshi ni chachu kwa ukuaji uchumi wa nchi yetu.”
Amesema
 uwezeshaji wa uchumi jumuishi ni msingi wa kuhakikisha kunakuwa na 
ustawi endelevu kwa watu wote, ambapo Serikali imeandaa Dira ya 
Maendeleo ya Taifa ya 2025 ambayo pamoja na mambo mengine imeainisha 
mazingira wezeshi yatakayowezesha nchi kunufaika kiuchumi, kijamii, 
kisiasa na kiutamaduni.
Mheshimiwa Majaliwa amesema Dira ya 
Maendeleo ya Taifa ya 2025 pia imelenga kuhakikisha kunakuwa na viwango 
vya juu vya maisha, amani na umoja, utawala bora na uchumi ulioimarika 
wenye ushindani katika jamii.
Pia, Waziri Mkuu amesema Serikali 
imeandaa sera mbalimbali ambazo zimelenga kuhakikisha kunakuwa na 
maendeleo endelevu na uchumi jumuishi. “Kati ya Sera hizo ni Sera ya 
Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004 ambayo ni Sera 
kiongozi kwenye masuala ya kuwezesha wananchi kiuchumi, sera hiyo 
imeweka mikakati inayolenga kuhakikisha kwamba Watanzania wanashiriki 
kikamilifu katika uchumi wa nchi”.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionesha  kitabu cha Taarifa ya 
Utekelezaji wa  Sera ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya Mwaka 2004 kwa 
Mwaka 2020/21 baada ya kuizindua katika Kongamano la Tano la Uwezeshaji 
Mwananchi Kiuchumi  kwenye ukumbi wa Jengo la PSSSF Makole jijini Dodoma

Waziri
 Mkuu, Kassim Majaliwa pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa katika picha
 ya pamoja na wadhamini wa Kongamano la Tano la Uwezeshaji Mwananchi 
Kiuchumi baada ya kufungua kongamano hilo  kwenye ukumbi wa Jengo la 
PSSSF Makole jijini Dodoma, Oktoba 5, 2021.  Kulia kwake ni Waziri wa 
Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji), Geofrey Mwambe.(Picha na Ofisi 
ya Waziri Mkuu)
 
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Kongamano la Tano la Uwezeshaji Mwananchi Kiuchumi kwenye ukumbi wa Jengo la PSSSF Makole jijini Dodoma.

Baadhi ya washiriki wa Kongamano la Tano la Uwezeshaji Mwananchi Kiuchumi wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua kongamano hilo kwenye ukumbi wa Jengo la PSSSF Makole jijini Dodoma

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akibonyeza kitufe wakati alipozindua Kanzidata ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi baada ya kufungua Kongamano la Tano la Uwezeshaji Mwananchi Kiuchumi kwenye ukumbi wa Jengo la PSSSF Makole jijini Dodoma, Oktoba 5, 2021. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Geofrey Mwambe na kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Beng’i Issa
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment