Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV
SERIKALI
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzanoa leo imetimiza ahadi zake
zilizotolewa na Rais wa Samiah Suluhu Hassan kwa kupeleka vifaa tiba
katika Hospitali ya Wilaya ya Chalinze mkoani Pwani.
Vifaa hivyo
vina thamani ya Shilingi Milioni 480 ikiwemo mashine ya Kupiga picha za
Mionzi yaani X-Ray, Jokofu la kuhifadhia maiti, mashine za kupimia damu
na vifaa mbalimbali.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa kwa vifaa
hivyo Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ameishukuru Serikali
kwa kutekeleza ahadi hii ndani ya muda wa wiki tatu toka kutolewa kwa
ahadi.
Wananchi wa Kata hiyo wakiongozwa na wakina mama ambao
walikuwa ipokea wameshangilia na huku wazee wakimuombea Mungu amlinde
Rais wa nchi yetu.
No comments:
Post a Comment