MKUU
wa Mkoa wa Pwani ,Abubakar Kunenge amemuagiza mkandarasi anayejenga
daraja la Mbuchi ,wilaya ya Kibiti kuharakisha ujenzi ili kuwaondolea
kero wananchi wanayoipata kwa sasa.
Kunenge
aliyasema hayo ,alipokuwa kwenye ziara ya Kamati ya siasa ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) mkoa huo ilipokuwa ikikagua miradi ya maendeleo likiwemo
daraja hilo la Mbuchi
Kunenge
alisema kukamilika kwa daraja hilo kutafungua njia kwa wakazi wa Vijiji
vya Mbwela ambao wanasafirisha bidhaa kwenda Muhoro na maeneo mengine
ya Wilaya ga Rufiji.
Mkuu
huyo wa Mkoa alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia
Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya maendeleo ambayo
inaondoa kero kwa wananchi.
Kaimu
Mhandisi Mkazi wa Mradi huo Mtani Silasi alisema mradi huo utatekelezwa
kwa miezi 12 na kwamba hadi kukamilika utagharimu kiasi cha shilingi
Bilion 6.1.
No comments:
Post a Comment