Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema serikali ya Mapinduzi Zanzibar itaendeleza Ushirikiano na uhusiano wake na Msumbiji katika adhma ya kuwajengea mustkbali mzuri wananchi wa pande zote mbili.
Mhe. Hemed alieleza hayo Ofisini kwake Vuga alipokutana na kufanya mazungumzo na balozi mdogo wa Msumbiji aliopo Zanzibar.
Alisema, kuna kila sababu ya kuendeleza ushusiano kati ya Zanzibar na Msumbiji uliodumu kwa muda mrefu sasa kutokana na muingiliano wa watu unaosababishwa na harakati mbali mbali za kimaisha ikiwemo Biashara.
Makamu wa Pili wa Rais alieleza kuwa, wapo wazanzibar wengi wanaoendesha maisha yao Nchini Msumbiji kutokana na ushirikiano mwema uliojengwa miaka mingi iliopitwa.
Mhe. Hemed alimueleza Balozi AGOSTINO ABACAR TRINTA kuwa Zanzibar kuna fursa nyingi zinazopatikana akitolea mfano sekta ya utalii na bidhaa zitokanazo na masuala viungo (Spices).
Nae, Balozi mdogo wa msumbiji anaefanya kazi zake Zanzibar
AGOSTINO ABACAR TRINTA Alimuhakikishia Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba Nchi ya Msumbiji itaendelea kushirikiana
na kufanya kazi zake kwa karibu na serikali ya mapinduzi Zanzibar na Tanzania
kwa ujumla kwa lengo la kuimarisha Diplomasia.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akimueleza
Balozi mdogo wa Msumbiji aliefika Afisini kwake Vuga AGOSTINO ABACAR TRINTA juu ya fursa zinazopatikana Zanzibar
kupitia sekta ya utalii na bidhaa zitokanazo na Viungo (Spices).
No comments:
Post a Comment