HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, July 31, 2021

RC KUNENGE AWAONGOZA WANANCHI MKOA WA PWANI KUCHANJA CHANJO DHIDI YA UVIKO 19 MJINI KIBAHA

 

 

 MKUU wa mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amepata chanjo ya UVIKO 19 leo Julai, 30 2021. Akichanjwa chanjo hiyo katikà viwanja vya kituo cha Afya Mkoani, kilichoko Kibaha Mjini, Mhe. Kunenge amewaasa Wanachi wa Mkoa huo kuwa ugonjwa upo na kuwataka kuchukua tahadhari wakati wote, amewataka Kuvaa barako, kunawa mikono kwa maji tiririka na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima.

Amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuonyesha njia kwa kupata chanjo. "nimechanja kwa hiari yangu mwenyewe mpaka sasa najisikia vizuri sijaona shida yeyote," alisema RC KUNENGE na kuongeza......Wananchi waje wachanje kwa hiari yao tunachotafuta ni salama tumepata chanjo kidogo tunaendelea kuratibu upatikanaji wa nyingi zaidi na tutaitoa bila usumbufu na bila malipo. "Chanjo hii kwa sasa itatolewa kwa makundi ya Kipaumbele kama vile watoa huduma ya afya, watu wenye umri kuanzia miaka 50 na kuendelea kama ambavyo muongozi wa Wizara ya Afya kuhusu Chanjo hiyo unavyosema.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, akichanjwa Chanjo dhidi ya Uviko 19 leo Julai 30, 2021 ikiwa ni uzinduzi wa Chanjo hiyo kwa wananachi wa Mkoa huo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad