Na. Josephine Majura, WFM, Arusha
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Bw.
Emmanuel Tutuba, ametoa wito kwa Wahariri nchini kuendelea kutoa elimu
kwa umma kuhusu masuala ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi
(PPP) ili waweze kutumia fursa zilizopo ili kushiriki katika utekelezaji
wa miradi ya maendeleo.
Alitoa wito huo wakati akifungua semina
ya siku 2 kwa Wahariri kutoka Vyombo mbalimbali vya Habari nchini
iliyofanyika jijini Arusha, ambapo amewataka Wahariri hao kuzisema fursa
zilizopo ili kutoa nafasi kwa wawekezaji kuweza kushirikiana na
Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa njia ya ubia ili kuboresha
huduma za jamii.
’’Serikali imeandaa programu ya PPP nchini ili
kuwezesha Sekta Binafsi kushirikiana na Serikali kuhakikisha inatekeleza
miradi ya maendeleo iliyopo katika Sekta mbalimbali," alisema Tutuba.
Alisema
Wizara ya Fedha na Mipango itaendelea kushirikiana na vyombo mbalimbali
vya Habari ili kuhakikisha wananchi wanapata elimu nzuri kuhusu
masuala ya ubia kwa kuwa wakiwa na uelewa sahihi wengi watavutiwa
kushirikiana na Serikali katika kutekeleza miradi mbalimbali nchini na
kufanya uchumi wa nchi kupanda.
Bw. Tutuba, amesema kuwa Serikali
inaendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini ili kuvutia
wawekezaji kwa kuwa miradi mingi inahitaji wawezekaji kama vile miradi
ya barabara, reli pamoja na madaraja.
Kwa upande wake Kamishna wa
Idara ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Dkt. John Mboya,
alisema kuwa utaratibu wa ubia wa Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ni njia
muhimu sana ya vyanzo mbadala vya kugharamia miradi ya maendeleo kwa
kuwa mapato ya Serikali pekee hayatoshi kugharamia miradi ya maendeleo.
“Serikali
imetunga Sera ya PPP ya Mwaka 2009, Sheria ya PPP Sura 103 na Kanuni za
PPP za Mwaka 2020 ili kuweka mazingira wezeshi ya kuishirikisha Sekta
Binafsi kwa utaratibu huo wa PPP”, alisisitiza Dkt. Mboya.
Aliongeza
kuwa hadi mwezi Mei, 2021 jumla ya miradi 41 kutoka Sekta ya
Mawasiliano, Ujenzi, Afya, Elimu, Biashara na Maji ipo katika hatua
mbalimbali za maandalizi, ikiwa na makadirio ya thamani ya sh. Trilioni
3.042.
Naye Mwenyekiti wa Mkutano huo wa Wahariri Bw. Ben
Mwangónda aliipongeza Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuendelea kufanya
semina mbalimbali kuhusu majukumu ya Wizara kwa kuwa semina hizo
zimewajengea uwezo kwenye taaluma zao katika kutoa taarifa kwa ufanisi
kwa wananchi kama ilivyokusudiwa.
Aliahidi kuwa kwa niaba ya
Wahariri walioshiriki semina hiyo atahakikisha vyombo vya Habari vinatoa
elimu mbalimbali kuhusu masuala ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta
Binafsi ili kuwawezesha wawekezaji kuongezeka nchini kwa kuwa elimu
inahitajika kwa jamii.
Semina ya Wahariri inafanyika kwa 2 mbili
mkoani Arusha ambapo imejumuisha jumla ya Wahariri 38 kutoka vyombo
mbalimbali vya Habari nchini ikiwa ni mwendelezo wa Semina
zinazoratibiwa na Wizara ya Fedha na Mipango kupitia Kitengo cha
Mawasiliano Serikalini ili kuwajengea uwezo wahariri na wanahabari kwa
ujumla kuhusu majukumu ya Wizara hiyo.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Bw.
Emmanuel Tutuba akizungumza na wahariri wa vyombo vya Habari wakati
akifungua semina ya siku 2 kwa wahariri hao kuhusu masuala ya Ubia kati
ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ambapo ametoa wito kwa wahariri hao
kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya ubia, Jijini Arusha.
Kamishina
wa Idara ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi Dkt. John Mboya
akizungumza wakati wa semina ya Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu
masuala ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, jijini Arusha.
Meza
Kuu, ikiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji
Mkuu wa Serikali Bw. Emmanuel Tutuba (katikati) wakifuatilia mijadala
iliyokuwa ikiendelea wakati wa semina ya wahariri wa vyombo vya Habari
kuhusu kuhusu masuala ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi,
jijini Arusha.
Kamishina
Msaidizi wa Idara ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Bw.
Bashiru Taratibu akifafanua jambo wakati wa semina ya wahariri wa vyombo
vya Habari kuhusu masuala ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta
Binafsi, jijini Arusha.
Maafisa
kutoka Idara ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, Bw.
Agustino Saibuli na Bi. Mwanaidi Araba wakifutalitia mijadala iliyokuwa
ikiendelea wakati wa semina ya Wahariri wa Vyombo vya Habari kuhusu
masuala ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, jijini Arusha.
John
Bukuku mhariri Mkuu wa Blogu ya Fullshangwe akichangia mada wakati wa
mijadala iliyokuwa ikiendelea wakati wa semina ya wahariri wa vyombo vya
Habari kuhusu kuhusu masuala ya ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta
Binafsi, jijini Arusha.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Bw.
Emmanuel Tutubaakizungumza na wahariri wa vyombo vya Habari wakati
akifungua semina ya siku 2 kwa wahariri hao kuhusu masuala ya ubia kati
ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ambapo ametoa wito kwa wahariri hao
kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya ubia, Jijini Arusha
Mwenyekiti
wa Mkutano wa Wahariri Bw. Ben Mwangónda, akitoa neno la shukrani kwa
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali
Bw. Emmanuel Tutuba (kushoto) baada ya kufungua semina ya wahariri hao
jijini Arusha.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Mlipaji Mkuu wa Serikali Bw.
Emmanuel Tutuba (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wahariri wa
vyombo vya Habari walioshiriki semina ya siku 2 kuhusu masuala ya Ubia
kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, jijini Arusha.(Picha na Wizara
ya Fedha na Mipango – Arusha).
Thursday, June 3, 2021
KATIBU MKUU: TANGAZENI FURSA ZILIZOPO KWA WELEDI KUVUTIA WAWEKEZAJI NCHINI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment