HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, May 21, 2021

Serikali yasisitiza Kuendelea Kushirikiana na Sekta zenye tija kwa Taifa

 

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dr.Leonard Akwilapo na Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Profesa Zacharia Mganilwa akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Wadau wa Sekta ya Usafirishaji. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 21, 2021 Mkoani Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji (NIT), Profesa Zacharia Mganilwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kamati ya Ushauri wa Wadau wa Sekta ya Usafirishaji katika mkutano uliofanyika leo Mei, 21,2021 Mkoani Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dr.Leonard Akwilapo akizungumza wakati wa uzinduzi wa kamati katika mkutano uliofanyika leo Mei, 21,2021 Mkoani Dar es Salaam.

Picha ya pamoja.



SERIKALI yasisitiza Kuendelea Kushirikiana bega kwa bega na Sekta zenye tija kwa Taifa.

Akizungumza Mara baada ya Kufungua rasmi Kamati ya Ushauri wa Wadau wa Sekta ya Usafirishaji Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Leonard Akwilapo iliyofanyika Dar es salaam amesema Serikali imeridhika na utendaji wa kazi unaofanywa na chuo Cha Usafirishaji nchini (NIT).

"Ni chuo pekee ambacho tunaendelea kuona wataalam wakizalishwa siku Hadi siku kutokana na progamu zinazotolewa nakupatikana wahitimu hatimae hao hao wanakua wataalam hivyo kwa namna moja au nyingi inasaidia Serikali kutotumia pesa nyingi kutafuta wataalam wakigeni badala yake wazawa wanaimarishwa na kuwa wataalam wabobezi."

Hata hivyo ameeleza Malengo ya Serikali katoka kusaidia chuo hicho ni pamoja na kutoa Mafunzo ya kinadharia yatakayokidhi Mahitaji ya nchi katika sekta ya Usafirishaji.

Vilevile amesema kutokana na Sekta hiyo ya Usafirishaji Kuendelea Kupanuka ataimarisha na kununua Meli pamoja na ndege.

Pia amewataka wanakamati hiyo waweze kujadili Mambo yatakayowezesha Chuo hicho Kupiga hatua ya Kimaendeleo ili Kusaidia Sekta ya Uchukuzi.

Kwa Upande wa Mkuu wa chuo hicho Pro. Zacharia Mganilwa amesema Kuna baadhi ya Miradi inaendelea Kutekelezwa ikiwemo Kujenga Majengo 9 na katika Kampasi yatajengwa Majengo matano.

"Majengo mengine ambayo tulitegemea yangekaamilika ni pamoja na Uwanja wa ndege kwa Dar es salaam Kwa ajili ya Wanafunzi kufanya Nadharia na kutokana na changamoto imepelekea ujenzi huo kuchelewa tunategemea hivi punde utaanza rasmi."

Mbali na ujenzi ametaja Mitaa mitano mipya ambayo tayari imeshadahili Wanafunzi na kupata ithibati kutoka Nacte.

"Miongoni mwa Mitaala hiyo ni pamoja na Uhandisi katika Reli ya Kisasa (SGR)".

Ameomba Mashirika ambayo Wanafunzi watafika Kama sehemu ya Mazoezi yani Mafunzo kwa vitendo waendelee kutoa Ushirikiano.

"Baadhi ya Wanafunzi tayari wameshahudhuria Mafunzo kwa vitendo sehemu mbalimbali Kama Latra, TLC, Sumatra kwa takribani Mwezi mmoja hivyo ningependa kuwasihi watoe Ushirikiano wadhati katika Hilo kusudi tuwapatie Wanafunzi wetu Elimu ya Usafirishaji katika kila nyanja "

Pia ameweka wazi kuwa kuna watumishi 8 wako nchini za Uingereza, Singapore pamoja na China wenye Shahada ya uzamivu Wamepelekwa huko Kwa ajili ya kuendelea na masomo.

"Serikali ina nia ya dhati kuzalisha wataalam kutoka nchini kwetu ambao tutajivunia kuwa nao hivyo tumeona ipo fursa ya kupeleka watu ambao baadae wataendelea kuzalisha wataalam wengine."

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad