HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, April 27, 2021

Waziri Jafo awasilisha Hotuba ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 bungeni jijini Dodoma

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo amesema Serikali kwa kushirikiana na mamlaka husika itaandaa Mkakati wa udhibiti wa athari za zebaki kwa afya ya binadamu na mazingira.

Jafo amesema hayo leo Aprili 27 wakati akiwasilisha Hotuba ya Mapato na   Matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 bungeni jijini Dodoma.

Alisema sambamba na hayo itaainisha na kufanya tathmini ya maeneo yenye shughuli nyingi za uchimbaji mdogo wa dhahabu kwa kutumia zebaki na kuweka mikakati ya kuyarejesha katika hali yake ya asili.

Aidha, waziri huyo aliongeza kuwa katika kutekeleza Mpango-kazi wa Taifa wa kupunguza matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu nchini Serikali itatoa mafunzo kwa mamlaka zinazohusika na udhibiti wa zebaki kuhusu namna ya kudhibiti uingizaji, matumizi na utupaji wa taka zitokanazo na zebaki nchini.

Katika hotuba hiyo pia alisisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kwa kuandaa Mkakati wa Nishati Mbadala ya Kuni na Mkaa kwa ajili ya kupikia na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi ya nishati mbadala.

“Mheshimiwa Spika tutaendelea kutoa elimu ya nishati mbadala hususan hususan kwa taasisi zinazotumia kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia zikiwemo magereza, polisi, na taasisi za elimu. Katika kipindi hiki, Ofisi itaendelea na ufuatiliaji wa utekelezaji wa mipango iliyowekwa na taasisi mbalimbali kuhusu matumizi ya nishati mbadala,” alisema.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mhe. Eric Shigongo alishauri Ofisi ya Makamu wa Rais ishirikiane na Ofisi ya Mkemia Mkuu kudhibiti uingizwaji wa zebaki nchini.

Katika hotuba hiyo aliyoiwasilisha kwa niaba ya Mwenyekiti Mhe. David Kihenzile alishauri Serikali itafute teknolojia mbadala ambayo wachimbaji hao wataitumia ili kuachana na matumizi ya zebaki.

“Uingizaji holela na utumiaji wa kemikali ya Zebaki nchini kutokana na kuwapo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu wanotumia kemikali hiyo, unaathiri kwa kiasi kikubwa afya na usatwi wa wchimbaji hao. Madhara ya matumizi ya kemikali hiyo yanatokana na wachimbaji wengi kuitumia bila ya kuwa nyenzo za kujinga kutokana na zebaki,” alisema.

Shigongo ambaye pia ni Mbunge wa Buchosa alitahadharisha kuwa maji yanayotumika kusafishia dhahabu yakiwa yamechanganyika na Zebaki, yanatiririkia kwenye vyanzo vya maji na kuwa watu wanapotumia maji hayo.

Naye Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Hawa Mchafu alishauri Serikali itumie fedha kutoka mifuko ya mazingira kwa kusaidia katika kujenga uelewa wa kupunguza matumizi ya zebaki.

Pia Mbunge huyo alipendekeza njia mbadala ya matumizi ya zebaki na kusema kuwa kemikali hiyo ina athari kubwa kwa binadamu hususan katika maeneo ya Kanda ya Ziwa ambako kuna shughuli za uchimbaji wa dhahabu.


6.6 Matumizi ya kemikali hatarishi – Zebaki
Mheshimiwa Spika, uingizaji holela na utumiaji wa kemikali ya Zebaki nchini kutokana na kuwapo kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu wanotumia kemikali hiyo, unaathiri kwa kiasi kikubwa afya na usatwi wa wchimbaji hao. Madhara ya matumizi ya kemikali hiyo yanatokana na wachimbaji wengi kuitumia bila ya kuwa nyenzo za kujinga kutokana na zebaki. Vilevile, maji yanayotumika kusafishia dhahabu yakiwa yamechanganyika na Zebaki, yanatiririkia kwenye vyanzo vya maji kama vile mito na mawaziwa. Watu wanapotumia maji kutoka vyanzo hivyo vilivyochafuliwa na zebaki ya kuoshea dhahabu, huathirika kiafya na wakati mwingine kupata maradhi sugu yanayogharimu maisha yao.
Mheshimiwa Spika, Kutokana na hali hiyo, Kamati inashauri kuwa:-
i) Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira ishirikiane na Ofisi ya Mkemia Mkuu kudhibiti uingizwaji na zebaki nchini;
ii) usimamizi na uratibu matumizi ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wa dhahabu nchini
25

uendelezwe na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa pamoja na Ofisi ya Mkemia Mkuu; na
iii) Serikali itafute teknolojia mbadala ambayo wachimbaji hao wataitumia ili kuachana na matumizi ya zebaki.

6.7 Taarifa ya Hali ya Mazingira nchini
Mheshimiwa Spika, Kifungu 175 (1) cha Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 kinamtaka Mkurugenzi wa Mazingira kuandaa na kutoa taarifa juu ya Hali ya Mazingira nchini kila baada ya miaka 2 na kuiwasilisha Bungeni. Hata hivyo uzoefu unaonesha kuwa upo ugumu wa kutekeleza masharti hayo jambo lililosababisha kuwasilishwa kwa taarifa hiyo mwaka 2008, 2014 na 2019. Kwa sababu hiyo, taarifa ya kwanza, ya pila na ya tatu hazikuweza kuzingatia masharti ya kuwasilishwa baada ya miaka miwili. Kwa msingi huo, Kamati inashauri kuwa Serikali iandae mapendekezo ya marekebisho ya kifungu hicho kwa kuongeza muda wa kutoa ripoti kufikia miaka 5.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo akiwasilisha Hotuba Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 bungeni jijini Dodoma leo Aprili, 2021.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Selemani Jafo na Naibu Waziri katika Ofisi hiyo Mhe. Hamad Hassan Chande wakisikiliza michango ya wabunge mara baada ya Hotuba Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 bungeni jijini Dodoma leo Aprili, 2021.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad