Kamanda
wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa (kulia)
akizungumza na baadhi ya wananchi katika Kata ya Pangani Ilala jijini
Dar es Salaam waliojitokeza kwenye huduma za mkono kwa mkono maarufu
'Ones Stop Center' zilifofanyika eneo hilo.
Mkurugenzi
wa Program wa Fredrich Naumann Foundation for Freedom East Africa kwa
Tanzania na Kenya, Veni Swai (wa kwanza kulia) akizungumza na baadhi ya
wananchi katika Kata ya Pangani Ilala jijini Dar es Salaam. Kulia kwake
ni Mratibu wa One Stop Center katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Mkaguzi
Msaidizi wa Polisi, Dk Christina Onyango akifuatilia.
Kamanda
wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa (kulia)
akizungumza na baadhi ya wananchi katika Kata ya Pangani Ilala jijini
Dar es Salaam waliojitokeza kwenye huduma za mkono kwa mkono maarufu
'Ones Stop Center' zilifofanyika eneo hilo.
Kamanda
wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
akizungumza na baadhi ya wanahabari mara baada ya hafla hiyo.
KAMANDA
wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amewataka
wanaume wanaofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia katika familia zao
wajitokeze na kudai haki zao mbele ya sheria, badala ya kuendelea kukaa
kimya kwa kilea kinachodaiwa wanaona aibu huku wakizidi kuteseka.
Kamanda
Mambosasa ametoa wito huo juzi katika Kata ya Pangani Ilala jijini Dar
es Salaam alipokuwa akifunga awamu ya pili ya huduma za mkono kwa mkono
maarufu 'Ones Stop Center' zinazotembea kwa waathirika wa unyanyasaji na
ukatili wa kijinsia yaliyofanyika katika kata tisa za Mkoa wa Kipolisi
wa Ilala takribani kwa siku 18.
Pamoja
na hayo aliongeza kuwa vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya
wanawake na watoto na unyanyasaji watoto vikiwemo vya ubakaji,
ukeketaji, utumikishaji watoto na ndoa za utoto vinavyowanyima watoto
haki zao haviwezi kukubalika, kwani watoto hao ndio viongozi na wajenzi
wa taifa la kesho.
“Watoto
wa sasa ndio akina Rais Samia Suluhu wa kesho; ndio akina Lazaro
Mambosasa wa kesho; ndio madkatari na viongozi wa kesho hivyo, lazima
haki zao zilindwe na waendelezwe.” Hivyo, lazima Watanzania tuungane na
kusimama pamoja kuhakikisha wanawake na watoto wanalindwa ili kesho na
kesho kutwa, washike nafasi mbaimbali kutumikia taifa,” alifafanua
Kamanda Mambosasa.
Kamanda
Mambosasa aliipongeza taasisi ya Fredrich Naumann Foundation for
Freedom East Africa kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kufanikisha
huduma za mkono kwa mkono zinazotembea na kuahidi kuendelea kuunga mkono
na kusaidia kufanikiwa zaidi kwa huduma hizo ili kukomesha vitendo vya
unyanyasaji na ukatili wa kijinsia eneo lake.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Program wa Fredrich Naumann Foundation for
Freedom East Africa kwa Tanzania na Kenya, Veni Swai akizungumza katika
hafla hiyo, alilipongeza Jeshi la Polisi kwa jitihada za kupambana na
uhaifu ukiwemo ukatili wa kijinsia, na hasa utaratibu wa kuwafuata
wananchi mahali walipo pamoja na kutoa elimu na huduma dhidi ya ukatili
wa kijinsia.
Alisema hatua hiyo inaifanya jamii kuongeza imani yake kwa polisi hivyo, kujitokeza kueleza kero zao zikiwamo za kifamilia.
“Kitendo
cha polisi kuwafuata wananchi katika maeneo yao na kusikiliza kero zao
sambamba na kuwapa msaada ukiwamo wa kisheria, msaada wa kipolisi,
unasihi na huduma za afya na elimu dhidi ya ukatili wakijinsia,
kinaonesha uhusiano mwema baina ya polisi na raia unazidi kuimarika.
Bado wadau wote kwa pamoja tuna kazi kubwa mbele yetu na sisi tunaahidi
kuendelea kushirikiana na polisi kadiri inavyowezekana.” Alisema Bi.
Swai.
Naye
Mratibu wa One Stop Center katika Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Mkaguzi
Msaidizi wa Polisi, Dk Christina Onyango, alisema mbali na vituo hivyo
kutoa huduma za upimaji afya kama macho, sukari na shinikiza la damu,
unasihi, huduma za kisheria, pia wananchi wamekuwa wakifundishwa namna
ya kubaini, wahusika, dalili, aina na namna ya kuripoti na kutunza
ushadidi dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Baadhi ya wananchi wakihudumiwa kwenye huduma za mkono kwa mkono maarufu 'Ones Stop Center' zilifofanyika eneo hilo.
Huduma zikitolewa kwenye hafla hiyo.
No comments:
Post a Comment