Mkuu
 wa Wilaya ya Nyamagana Dkt Phillis Nyimbi ameongoza wananchi mbalimbali
 wanaoishi FCkatika Kata ya Lwanwima kupanda miti ya maparachichi katika
 Shule ya Msingi Lwanwima ikiwa ni sehemu ya kampeni ya wilaya hiyo 
kuzifanya shule zote za kijani.
Kulingana na maelezo ya Afisa 
Misitu wa wilaya hiyo, Deogratius Julius, kampeni hiyo inalenga kupanda 
miti katika shule za sekondari na msingi na hata katika maeneo ya 
taasisi za umma.
Hadi sasa wameshapanda miti 41,996 katika kipindi hiki cha mvua.
Wadau
 mbalimbali wa mazingira walishiriki zoezi hilo wakiwemo Aga Khan Healrh
 Services kupitia mradi wake wa Impact kanda ya ziwa ambao walikabidhi 
miche 280 ya maembe na maparachichi

Picha mbalimbali katika kampeni ya upandaji miti ya miparachichi katika wilaya ya Nyamagana.
 

 
 




 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment