Katibu Mkuu 
wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk.Leonard Akwilapo, 
ameipongeza Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii(CSSC),kwa mchango wake 
katika sekta ya elimu nchini huku akiahidi serikali kufanyia kazi maoni 
yanayotolewa ikiwamo kupunguza kwa mitihani ya majaribio.
Akifungua
 leo Mkutano wa mwaka cha Wakuu wa Shule za Sekondari na Msingi za 
makanisa, Dk.Akwilapo, amesema suala la mitihani ya majaribio lina utata
 na kudai kuwa ni mingi na wakati mwingine inaipa Wizara wakati mgumu 
kuiratibu.
“Kuna wengine wanadhani elimu inapatikana kwa kuuliza 
wanafunzi maswali mara kwa mara, ili ng’ombe anenepe ni kuhakikisha 
amekula na si kumpima uzito asubuhi, mchana na jioni, kitu kizuri ni 
kuimarisha ufundishaji,”amesema.
Ameongeza kuwa “Kuna dhana 
nyingine imeongezeka hadi kuweka kambi kufanyishwa mitihani kila siku 
hadi jumamosi,kuna mambo tumekemea na si sahihi kwamba ili mwanafunzi 
afaulu ni kupigwa mitihani, majaribio hatuyakatai bali kila mara 
inamchosha mtoto.”
Aidha, amesema nia ya serikali ni kutoleta 
mgongano na wanaendelea na majadiliano na kutaka kuimarisha ufundishaji 
na si kupewa mitihani kila siku.
Pia amezitaka shule kuzingatia maelekezo ya serikali katika kumkaririsha mwanafunzi darasa kwa kuwa suala hilo linalalamikiwa.
“Tunatambua
 mchango wenu mnaoutoa nchini katika sekta ya elimu, hata hivyo baadhi 
ya shule zisizo za serikali kama nyingine zipo kwenu au hazipo, ambazo 
zinaenda kinyume na maelekezo ya serikali, niwakumbushe myazingatie 
kukaririsha wanafunzi bila kuzingatia taratibu ni tatizo tunalokutana 
nalo sana,”amesema.
Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa Tume hiyo, 
Peter Maduki, amesema la mkutano huo ni kuweka mikakati ya utoaji huduma
 bora ya elimu na kuangalia kero zilizopo na kuzitafutia ufumbuzi.
“Pia
 tutajadili namna ya kuboresha huduma ya  TEHAMA itatusaidia sana katika
 kuboresha elimu na kupunguza gharama ya utoaji wa elimu na kuwapunguzia
 mzigo wazazi,”amesema.
Ameomba Wizara kuangalia namna ya 
kupunguza mitihani ya majaribio ambayo imeonekana kuendelea kuibuka 
mbali na inayopaswa kufanyika kitaifa.
“Kunaendelea kuibuka 
mitihani ya majaribio mara ya kikata, kiwilaya hali inayosababisha 
mwingiliano wa mitihani na hii hata inashusha ubora wa mitihani tunaomba
 umakini zaidi uwepo katika kuendesha mitihani,”amesema.


Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya 
Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC) Bw.Peter Maduki,akielezea jinsi 
wanavyotoa elimu katika shule zao wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa wakuu
 wa shule za Sekondari na Msingi za Makanisa yaliyo chini ya Kanisa 
Katoliki na Jumuiya ya Kikristo Tanzania ambayo yanaratibiwa na Tume ya 
Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC) iliyofanyika leo Januari 25,2021 
jijini Dodoma.
  
Sehemu ya washiriki wakifatilia Hotuba ya Mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa wakuu wa shule za sekondari na Msingi za Makanisa yaliyo chini ya Kanisa Katoliki na Jumuiya ya Kikristo Tanzania ambayo yanaratibiwa na Tume ya Kikristo ya Huduma za Jamii (CSSC)

No comments:
Post a Comment