HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 15, 2020

DAS LUDEWA ATOA AGIZO KWA MADIWANI JUU YA WANAFUNZI KURIPOTI SHULENI

 

 Na Shukrani Kawogo, Njombe.

Katibu tawala wa wilaya ya Ludewa Zaina Mlawa amewataka madiwani wote kuhakikisha kuwa mpaka kufikia January 30 watoto waliofaulu darasa la saba na kupangiwa shule wanaripoti katika shule walizopangiwa na kuanza masomo.

Hayo ameyasema katika hafla ya kuwaapisha madiwani iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya na kuongeza kuwa wasisubiri serikali itumie nguvu katika kufanikisha hili.

Amesema mara nyingi idadi ya wanafunzi waliofaulu na kupangiwa shule ni tofauti na idadi ya wanafunzi wanaripoti katika shule hizo kitu ambacho kinashusha ukuaji wa sekta ya elimu katika wilaya hiyo.

"Madiwa mkisimama vyema katika nafasi zenu mnaweza kuleta maendeleo ya elimu katika kata zenu na wilaya kwa ujumla, hivyo mhakikishe mnatekeleza hili kwa ushirikiano na wazazi", Alisema Mlawa.

Aidha kwa upande wa mbunge wa jimbo hilo Joseph Kamonga amewaomba madiwani hao kusimamia vyema vyanzo vya mapato pamoja na kubuni vyanzo vingine ili kukuza uchumi wa wilaya hiyo.

Aliongeza kuwa wanapaswa kukusanya mapato ili fedha hizo zitumike kutatua matatizo mbalimbali ikiwemo kuboresha sekta ya elimu na afya.

"Ndugu zangu tusipoweza kukusanya mapato hatutaweza kutatua changamoto za wananchi, hivyo tunapaswa kufanya hivyo  kwa nguvu zote na pale patakapotokea changamoto za kisera au Sheria Mimi simu yangu iko wazi muda wote msisite kunishirikisha", Alisema Kamonga.

Kwa upande wa mmoja wa madiwani hao Willbard Mwinuka amesema kuwa wameyapokea yote waliyoaswa na wakuu wa idara mbalimbali pamoja na mbunge na wataenda kutekeleza kwa kila hali ili kuleta maendeleo katika wilaya hiyo.

Alisema kwa upande wake amejipanga vyema katika kufanya kazi kwa bidii na atahakikisha analeta Maendeleo katika kata yake na wilaya kwa ujumla.

Bunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga akimpongeza Diwani wa Mawengi Leodga Mpambalioto kwa kupata ushindi wa kishindo katika nafasi ya naibu mwenyekiti wa halmashauri kwa ambapo ameshinda kwa asilimia mia moja.
Mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga (Aliyesimama) akiongea na Baraza la madiwani katika kikao cha kwanza baada ya kuapishwa. Kushoto ni Balozi Dk. Pindi Chana, kulia ni mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Sunday Deogratius, mwenyekiti wa halmashauri Wise Mgina na Mkuu wa mkoa wa Njombe Marwa Rubirya.
Mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga (kushoto) akiteta Jambo na mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Sunday Deogratius.
Viongozi mbalimbali wakiwasili katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa kwa lengo la kuwaapisha madiwani na kuanza kikao cha kwanza Cha Baraza. Kulia ni mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga, mbunge viti maalum Balozi Dk. Pindi Chana, mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Sunday Deogratius pamoja na Mkuu wa mkoa wa Njombe Marwa Rubirya.
Katibu tawala wa wilaya ya Ludewa Zaina Mlawa (Aliyesimama kulia) akiongea na madiwani hawapo pichani, katika halfa ya kuwaapisha madiwani iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri wilayani humo. Anayefuata ni mkuu wa mkoa wa Njombe Marwa Rubirya, mwenyekiti wa halmashauri Wise Mgina Pamoja na mkurugenzi wa halmashauri Sunday Deogratius.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa Sunday Deogratius akiteta jambo na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Wise Mgina. Kushoto ni mbunge wa jimbo la Ludewa Joseph Kamonga na kulia ni katibu tawala wa wilaya hiyo Zaina Mlawa na mkuu wa mkoa wa Njombe Marwa Rubirya.

Balaza la madiwani wilaya ya Ludewa pamoja na wageni waalikwa wakiwa wamesimama baada ya kuapishwa na kuchagua mwenyekiti wa halmashauri.
Mwenyekiti wa halmashauri wilaya ya Ludewa Wise Mgina akiwapa mikono meza kuu baada ya kupata ushindi wa nafasi hiyo kwa kura 32 Kati ya 35 zilizopigwa.
Baraza la madiwani wilaya ya Ludewa wakifiatilia majadiliano ya ajenda mbalimbali

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad