NA MWAMVUA MWINYI, PWANI
WAJUMBE
wa kikao cha bodi ya barabara mkoani Pwani ,wameazimia kuiomba Serikali
kuangalia namna ya kuunganisha wakala wa barabara (TANROADS ) na TARURA
na kuwa chini ya Wizara moja ili kuboresha huduma za mjini na vijijini
ama kuongeza mgawanyo wa fedha kwa TARURA kutoka asilimia 30 na kufikia
asilimia 40.
Mabadiliko
hayo yatasaidia TARURA kuongeza ufanisi wa kutatua changamoto ya ubovu
wa miundombinu ya barabara na kuboresha barabara hasa maeneo ya vijijini
ambapo wananchi wanapata kero zaidi.
Akizungumza
wakati akifunga kikao hicho,mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist
Ndikilo alieleza, TARURA inapaswa ipewe nguvu kwa kuongezwa fedha za
utekelezaji kutoka asilimia 30 hadi 40 na TANROADS itoke kwenye asilimia
70 na kuwa 60 ili kuiongezea ufanisi TARURA.
"TANROADS inafanya kazi kubwa na TARURA inafanya kazi kubwa lakini kwasasa TARURA inahemewa na barabara nyingi za vijijini huku ikiwa na bajeti ndogo ya utekelezaji .
"TANROADS inafanya kazi kubwa na TARURA inafanya kazi kubwa lakini kwasasa TARURA inahemewa na barabara nyingi za vijijini huku ikiwa na bajeti ndogo ya utekelezaji .
Aidha
TARURA inashindwa kupandisha hadhi baadhi ya barabara zake kwani ni
lazima ipige hodi kwa waziri mwenye dhamana anaeshughulika na TANROADS .
"Utekelezaji
wake ni mgumu kidogo ,wanakwama kiutendaji ,huku wananchi wa vijijini
wakiendelea kupata shida na wakibakia kuziba mashimo na kufanya
ukarabati zaidi kuliko kujenga barabara mpya kutokana na bajeti ndogo"
alieleza Ndikilo.
Mbunge
wa jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete alisema ,jimbo la Chalinze ni
miaka minne mfululizo haijabahatika miradi inayotekelezwa kwa fedha za
TARURA .
Kutokana na hilo
,mkuu wa mkoa Ndikilo alielekeza apelekewe taarifa ya ufafanuzi wa kila
halmashauri ,jumla ya miradi mipya na ya zamani ,mgawanyo wa fedha ili
kujiridhisha.
Mkuu wa
wilaya ya Mkuranga,Filberto Sanga aliomba Serikali kuangalia namna ya
kuunganisha wakala hizo ama kuiongezea fedha TARURA kwani kipindi
kilichopita wakulima wa korosho walishindwa kufikisha korosho zao
barabarani kutokana na barabara za vijijini kuwa mbovu .
Nae
meneja wa TANROADS Mkoani Pwani, Yudas Msangi alieleza bajeti ya mwaka
wa fedha 2020/2021 ni bilioni 35.318 ambapo bilioni 24.297 ni ya
matengenezo na bilioni 11.021 ni ya miradi ya maendeleo.
Alifafanua
pia ,tatizo walilonalo ni fedha kushindwa kusainiwa kwa wakati hivyo
fedha zinachelewa na kushindwa kutekeleza majukumu yao .
Hata
hivyo alibainisha,wananchi wanadai fidia ya bilioni 57 ,ambako
wanatakiwa wapishe ujenzi wa barabara mbalimbali katika mkoa huo.
Kwa
upande wake TARURA Mkoa bajeti ni bilioni 11.243 ambapo matengenezo ni
bilioni 6.993, huku bilioni 2.95 miradi ya maendeleo na bilioni 1.3
miradi maalum.
No comments:
Post a Comment