*Jitihada za JPM zatajwa kuchochea ukuaji wa sekta ya fedha.
IMEELEZWA
kuwa utendaji na uongozi madhubuti wa Rais Dkt. John Joseph Magufuli
katika kuweka mikakati na mazingira wezeshi, shirikishi na endelevu
kisera imechochea ukuaji wa sekta ya fedha hususani katika masoko ya
mitaji na uchumi kwa ujumla nchini.
Hayo yameelezwa na Afisa
Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) CPA
Nicodemus Mkama leo jjini Dar es Salaam wakati wa hafla ya kuorodheshwa
kwa hisa za JATU Plc katika soko la hisa la Dar es Salaam
(DSE.)"Nawashukuru wadau wa sekta ya fedha kwa kuhudhuria hafla hii ya
kuorodheshwa kwa hisa za Kampuni ya JATU Plc kwenye soko la hisa la Dar
es Salaam, huu ni uthibitisho kwamba sekta ya fedha ina wadau wengi
wanaounga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais
Magufuli iliyoweka mazingira wezeshi na kiutendaji yenye malengo ya
kukuza uwekezaji kupitia masoko ya mitaji." Ameeleza.
Amesema
kuwa, hisa zapatazo 2,164,349 kutoka Kampuni ya JATU Plc zimeorodheshwa
katika soko la hisa leo na hiyo ni kutokana na matokeo chanya ya elimu
na ufahamu waluoupata viongozi waanzilishi wa JATU Plc ambao ni vijana
wa kitanzania waliotumia fursa hiyo baada ya kushiriki shindano la
masoko ya mitaji kwa wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu
nchini.
Aidha ameeleza, Serikali kupitia Mamlaka ya Masoko ya
Mitaji na Dhamana (CMSA) itaendeleza majukumu yake ya kusimamia,
kuratibu na kuendeleza sekta ya masoko ya mitaji hapa nchini.
"Sekta
hii husaidia Kampuni katika upatikanaji wa mitaji kwa muda mrefu na
kuorodheshwa kwa JATU Plc katika soko la hisa la Dar es Salaam ni
matokeo chanya ya kufanikisha azma ya Serikali ya awamu ya tano katika
kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa mitaji kwa wakulima wadogo ili
kuongeza tija kwenye sekta ya kilimo na kuifanya sekta hiyo kuwa ya
biashara." Amesema.
Pia ameipongeza JATU Plc kwa kujidhatiti kwa
kuwekeza katika sekta mbalimbali pamoja na kutoa ajira zipatazo 10,650
wakiwemo wanawake kwa asilimia kubwa na kuwahimiza kuendelea kufanya
kazi kwa uaminifu ili kuweza kufikia azma ya maendeleo.
Vilevile
ameielekeza bodi ya Wakurugenzi na uongozi wa Kampuni ya JATU
kuhakikisha kunakua na ongezeko la thamani katika uwekezaji wao ili
waweze kunufaika kiuchumi ikiwemo kupata gawio la faida.
Kwa
upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE,)
Moremi Marwa amesema, Kampuni ya JATU Plc imeorodhesha hisa zake 2,164,
349 zenye ukubwa wa mtaji wa thamani ya shilingi bilioni moja na milioni
83.
Amesema, malengo kwa kuorodhesha hisa za JATU ni kuwezesha
wanahisa wa JATU Plc kuendelea kununua na kuuza hisa zao katika bei
inayoamuliwa na soko.
"Ninaupongeza uongozi wa JATU kwa kufikia
hatua hii na kuwapa imani Wana hisa wake kupitia shughuli wanazozifanya
ikiwemo kilimo na masoko, hii ni hatua kubwa katika kuelekea
maendeleo...Tunaamini kupitia hatua hii ajira zitazalishwa kwa wingi
pamoja na kuongeza pato la Serikali kupitia kodi." Ameeleza.
Amesema
Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA,) imekuwa ikishiriki
katika kuzileta sokoni kampuni za namna hiyo, na hadi leo Kampuni 28
ikiwemo JATU zimeorodheshwa huku Kampuni 27 zilizoorodheshwa awali
zikiwa na ukubwa wa mtaji wa thamani ya shilingi trilioni 15, huku
trilioni 9.1 zikitokana na kampuni za ndani.
Naye Ofisa
Mtendaji Mkuu wa JATU Peter Isare, alisema kampuni hiyo inayomilikiwa na
wanawake,vijana pamoja na watu wa kipato cha kati, wamejiunga pamoja na
kushirikiana katika miradi mikubwa ya kilimo, viwanda, masoko na
Tehama.
Alisema hadi kufikia mafanikio hayo ya kusajiliwa soko la
hisa, wameweza kuanzisha mashamba katika hekari zipatazo 17,678
yaliyopo katika mikoa mbalimbali hapa nchini ikiwemo Tanga, Manyara,
Singida,Ruvuma,Morogoro na Njombe.
Alisema hatua ya kampuni hiyo
kuorodheshwa katika soko la hisa kutazidi kuiwezesha kushiriki katika
miradi mikubwa zaidi na hivyo kuisaidia kubadirisha maisha ya maelfunya
watanzania.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA)
CPA Nicodemus Mkama (wa tatu kulia) akipiga kengele kuashiria
kufunguliwa kuanza kuuzwa kwa hisa za kampuni ya JATU PLC katika Soko la
Hisa la Dar Es Salaa (DSE),kwenye hafla fupi ya kuorodheshwa kwa hisa
za Kampuni ya JATU Plc katika soko la hisa la Dar es Salaam (DSE.)
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA)
CPA Nicodemus Mkama akizungumza mbele ya Waandishi wa habari na Wageni
waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo leo jijini Dar es
Salaam, wakati wa hafla fupi ya kuorodheshwa kwa hisa za JATU Plc katika
soko la hisa la Dar es Salaam (DSE.)Baadhi ya Wageni waalikwa wakifuatilia hafla hiyo fupii iliyofanyika leo jijini Dar
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE,) Moremi Marwa
akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari na wageni waalikwa waliofika
kwenye hafla fupi ya kuorodheshwa kwa hisa za Kampuni ya JATU Plc kwenye
soko la hisa la Dar es Salaam
Mtendaji
Mkuu wa Kampuni ya JATU Plc Peter Isare akizungumza mbele ya Waandishi
wa Habari na Wageni waalikwa mbalimbali wakati wa kampuni hiyo
ikiorodheshwa kwenye soko la hisa la Dar es Salaam,Isare alisema kuwa
kampuni hiyo inamilikiwa na wanawake,vijana pamoja na watu wa kipato cha
kati, wamejiunga pamoja na kushirikiana katika miradi mikubwa ya
kilimo, viwanda, masoko na Tehama.
Monday, November 23, 2020

KAMPUNI YA JATU PLC YAORODHESHWA KWENYE SOKO LA HISA LA DAR ES SALAAM
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment