Karibu wa CCM Wilaya ya Longido Joseph Olesadira
Mogombea ubunge kwa tiketi ya CCM akizungumza na wananchi wa kata ya Longido Mjini na ile ya orbomba katika mkutano wa hadhara uliofanyika Longido
Mwenyekiti
wa CCM wilaya ya Longodo Joseph Olesadira akizungumza na wananchi wa
Jimbo la Longido katika mkutano wa hadhara u;liofanyika jana na
kushirikisha kata mbili ya Longodo
Katibu wa CCM Wilaya ya Longido Ezekilel akizungumza na wananchi wa kata ya Longido Mjini na ile ya orbomba katika mkutano wa hadhara uliofanyika Longido
Wananchi wa kata ya
Longido Mjini na ile ya orbomba katika mkutano wa hadhara uliofanyika
Longido wakisikiliza sera za wagombea ubunge na udiwani katika jimbo
hiloWananchi wa kata ya
Longido Mjini na ile ya orbomba katika mkutano wa hadhara uliofanyika
Longido wakisikiliza sera za wagombea ubunge na udiwani katika jimbo
hiloMgombea ubunge kwa tiketi ya CCM Longido Dkt.Stephen Kiruswa
amesema kuwa atakapochaguliwa katika Jimbo hilo kwa kushirikiana na
madiwani watahakikisha wanasimamia wazawa wanapata haki ya kumiliki
Ardhi, bila kuwasahau wanawake na kupata stahiki zao.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliyoandaliwa na Chama hicho kwa kata mbili za Longido mjini na Orbomba ,Kiruswa
alisema kazi ya kutafuta Viongozi siyo kazi rahisi bali ni jambo gumu
linalohitaji utayari kwaajili ya kuwatumia wananchi bila ubaguzi na
kutatua changamoto zao ambapo yeye amesema yupo tayari .
Dkt.Kiruswa
alisema kwamba kwa kushirikiana na madiwani katika Jimbo hilo mara
baada ya Uchaguzi watahakikisha wanasimamia vyema maslahi ya wanalongido
Ikiwemo miradi ya Afya,Maji ,Umeme,Elimu Ili kila mwananchi afaidike na
miradi hiyo.
Wakizungumza wajumbe wa kamati ya siasa wilaya ya Longido wakusema kuwa Dkt.John Pombe Magufuli
amekuwa mzazi wa watoto wao kuanzia darasa la kwanza hadi sekondari kwa
kuwapatia Elimu bure bila malipo na kusababisha watoto wao kung'ara
kielimu
Sambamba na hayo Kamati hiyo ulisema kuwa wamekuwa wanufaika wakubwa wa maji ya mto Simba kuwafikia Longido, ikiwa ni juhudi za Magufuli na kuepuka adha ya kwenda kutafuta maji nchi jirani ya Kenya kwenye visima,kwa Sasa wanatumia maji Safi na salama.
Akizungumzia changamoto iliyokuwepo awali ya Morani kujiandikisha na kuacha kupiga kura Diwani mteule kata ya Longido Thomas Ngobei
alisema kuwa tayari wameshaweka utaratibu nzuri wa zamu ya kwenda
machungani kwa awamu ili wengine wapate nafasi ya kupiga kura kama haki
yao ya msingi
Kwa upande wake katibu wa CCM wilaya ya Longido Ezekiel Mollel alisema
kichama wana kata 18 hivyo ujio wa mgombea Urais Taifa Dkt.Magufuli
Mkoani Arusha, alisema (w) hiyo wamejipanga ipasavyo kumpokea kwa
kishindo
Aidha
alimalizia kwa kuwataka wananchi wote kujitokeza kwa wingi siku ya
tarehe 28/10/2020 kwaajili ya kumpigia kura Rais ,Wabunge na Madiwani wa
chama cha mapinduzi kwani wananchi wenyewe wamejionea kwa macho
maendeleo katika wilaya hiyo na kwa Taifa kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment