HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, September 10, 2020

UJENZI WA BANDARI YA KISIJU UTATOA FURSA YA AJIRA KWA VIJANA NA KUINUA UCHUMI

IMEELEZWA kuwa ujenzi wa bandari ya kisiju utatoa fursa ya ajira kwa vijana na kuinua uchumi wanamkuranga na nchi kwa ujumla. 

Akizungumza na wananchi wa vijiji tatu vya kata ya kisiju  wakati wa kampeni  Abdalah Ulega amesema lengo lake ni kuona bandari inafanya kazi ili vijana waondokane na umaskini na wapate uchumi.

Aidha ulega amesema bandari hiyo ya kisiju ambayo imekufa kutokana na mikoko kuota na mchanga kujaa ilikuwa inapokea mashua 12 kwa cku lakini sasa inapokea mashua moja,nisuala linalomuumiza lakini anapambana liweze kufanikiwa. 

Ulega ameongeza kuwa ustawi wa kisiju ni bandari na barabara hivyo amewataka wananchi kuchagua chama cha mapinduzi ili kiweze kutatua changamoto zao. 

Sanjari na hayo ulega amesema mpaka sasa zahanati tano zimefungulia, tisa zimekamilika ikiwemo zahanati ya koma na ishrini na sita zipo katika hatua mbalimbali.

Aidha ulega amewataka wanachama wa chama cha mapinduzi kuondoa makundi baina yao na kuwa na umoja na mshikamano kuhakikisha wagombea wote wa chama cha mapinduzi kinashinda kwa kishindo. 

Hata hivyo Ulega amefanya kampeni katika vijiji vitatu vya kisiju, ambapo viwili vipo kisiwani ambavyo ni koma na kwale pamoja na kisiju pwani vilivyopo  kata ya kisiju .

Mgombea Ubunge jimbo la Mkuranga, Abdallah Hamisi Ulega (kushoto) akizungumza na wanachama wa Chama cha Mapindunzi na Wananchi wa kijiji Koma na Kwale kata ya Kisiju ambapo amewaomba wanachama wa chama cha mapinduzi kuondoa makundi baina yao na kuwa na umoja na mshikamano il kuhakikisha wagombea wote wa chama cha mapinduzi wanashinda kwa kishindo.leo  Septemba 09,2020 wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani. 

Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Mgombea Ubunge jimbo la Mkuranga, Abdallah Hamisi Ulega.

 


Mke wa Mgombea Ubunge Jimbo la Mkuranga koa wa Pwani ,Mariam Ulega(kulia) akiwasalimia wananchi kijiji Koma na Kwale kata ya Kisiju leo  Septemba 09,2020




Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mkuranga, Ali Msikamo(kusoto) akisisitiza jambo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad