HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 25, 2020

MAZIWA YA NG’OMBE NI KWAAJILI YA MTOTO WA NG’OMBE-DKT JESCAR LEBA

 

 Mganga mkuu wa halmashauri ya manispaa ya Iringa Dokta Jescar Leba amewataka wakinamama wanaojifungua kufuata maelekezo ya wataalamu ikiwemo kutowaongezea chakula chochote watoto pindi wanapozaliwa hadi kufikia umri wa miezi sita kwa lengo la kulinda afya zao.


Dokta Leba ametoa rai hiyo kwenye shughuli ya wakina mama wenye watoto chini ya miezi 6 ijulikanayo kama “Mother Meetup” iliyoandaliwa na na mradi wa USAID TULONGE AFYA kupitia jukwaa la NAWEZA kwa lengo la kuwakumbusha wakinamama hao juu ya malezi bora ya watoto ambapo amesema watoto wanaozaliwa hawapaswi kuongezewa chakula chochote kwakuwa nyongeza hiyo ya chakula inaweza kuathiri afya na ukuaji wao kimwili na kiakili.

Aidha Dokta leba ameongeza kuwa zipo mila na desturi mbaya zilikuwa zinaathiri kampeni hiyo lakini kwa juhudi za serikali na wadau wa maendeleo, jamii imeelewa umuhimu wa unyonyeshaji maziwa ya mama pekee na kuanza kufuata utaratibu huo na kuongeza kuwa kwa mujibu wa takwimu walizonazo kwasasa unyonyeshaji bila nyongeza ya chakula kwa miezi sita ni karibu asilimia mia moja

“Tulikuwa na changamoto ya mila na desturi katika eneo hili ambapo wazazi walikuwa wakishinikizwa na wanafamilia mfanobibi au majirani kwamba mtoto akilia anapaswa kupewa uji au hata maji kwa madai kuwa maziwa ya mama pekee hayatoshi lakini kwa sasa wengi wamekwishaelewa na utekelezaji ni karibu asilimia mia moja”. Aliongeza Dokta Leba

Baadhi ya wakinamama hao wametoa ushuhuda na kueleza kuwa changamoto ya mila na desturi ilikuwa kikwazo kutokana na jamii inayowazunguka kulazimisha watoto kupewa nyongeza ya chakula ndani ya muda mfupi wa kuzaliwa kwa madai kuwa maziwa yam am hayawezi kumtosheleza

“Mimi nilipojifungua ndani ya kipindi cha wiki mbili mtoto wangu wa kwanza alikuwa analia sana ndipo nikaambiwa nimuongezee chakula kwa madai kuwa maziwa yangu yalikuwa hayatoshi. Lakini nilikataa na kuendelea kumnyonyesha mwanagu mpaka alipofikisha miezi sita ndipo nikaanza kumuongezea vyakula na mpaka sasa ana afya njema”. alisema bi. Theresia Joseph ambaye ni mama wa watoto wawili

Sezaria Andrew ni yeye ni mratibu wa afya ya uzazi na mtoto wa manispaa ya Iringa alisema pamoja na hamasa iliyofanywa na serikali katika kuhakikisha unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee kwa kipindi cha miezi sita unazingatiwa, mchango wa wadau wa maendeleo kupitia miradi mbalimbali kama mradi wa USAID Tulonge Afya si wakubezwa katika mafanikio yaliyofikiwa kwenye kampeni hiyo.

“Tunawashukuru wadau wetu USAID TULONGE AFYA kwani wamekuwa kiungo cha mabadiliko ya tabia ndani ya jamii, ,tunawaomba waendelee kutuunga mkono ili tuendelee kumpambania mtoto wa kitanzania. Watoto wanaoanzishiwa chakula kabla ya miezi sita ya kuzaliwa wengi husumbuliwa na magonjwa mbalimbali ikiwemo magonjwa ya tumbo kutokana na utumbo kutokuwa na uwezo wa kuchakata chakula” alisema dokta Sezarina Andrew.

Mradi wa USAID Tulonge Afya ni mradi miaka mitano unatekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na shirika la FHI360 na wadau wengine wakiwamo mashirika ya TCDC na TMARC chini ya ufadhili wa shirika la kimarekani lijulikanalo kama USAID. Mradi huu unatekelezwa hapa nchini katika Wilaya 29 kwenye mikoa 12. Kwa upande wa mkoa wa Iringa mradi unatekelezwa katika wilaya tattu ambazo ni Iringa Manispaa, Mufindi DC na Kilolo DC. 

Mmoja wa akina mama waliohudhuria kongamano la onyonyeshaji linalojulikana kama Mother Meet Up event lililoandaliwa na USAID TULONGE AFYA mjini Iringa Pendo Muhongole akifuatilia kwa makini maelezo ya mgeni rasimi kwenye kongamano hilo.

Mgeni rasmi wa kongamano la unyonyeshaji linalojulikana kama Mother Meer Up event lililoandaliwa na USAID TULONGE AFYA mjini Iringa Dkt Jescar Leba (mganga mkuu wa halmashauri ya manispaa ya Iringa) akiongea na akinamama wakati wa kongamano hilo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad