Waziri
mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambaye pia Ni mjumbe wa kamati
kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kasimu Majaliwa amemtaka mkuu wa
Wilaya ya Monduli Edward Balele pamoja na Mkurugenzi wa halmashauri
hiyo Stephen Ulaya kukarabati haraka magari ya kubebea magonjwa matatu
ambayo yameharibika kwa sasa.
Akizungumza
wakati wa Ufunguzi wa kampeni za Ubunge katika Jimbo Monduli Majaliwa
alisema kuwa Serikali imetoa magari Hayo ili Kuhakikisha kuwa
wananchi,wanaletewa huduma za afya kwa katika vijiji hivyo Ni vyema
wanatengeneza mapema ili wananchi waweze kupata huduma.
Aidha
alisema kuwa Serikali ilileta magari ya kubebea wagonjwa matano lakini
amesikia magari mawili tu ndio yanafanya kazi kitu ,hivyo alimuagiza
mkurugenzi afanye haraka magari Hayo kukamilika .
Alisema
kuwa kila mtu anajua kazi zilizofanywa na Serikali inayoongozwa Chama
Cha mapinduzi ,katika kipindi Cha uongozi wa miaka mitano iliopita
Ambapo alisema kwa kutekeleza ilani ya Chama Cha mapinduzi ,Serikali
yetu imeweza kuleta maendeleo pamoja na kuing'arisha nchi yetu
"Tumeweza
kujenga vituo vya afya 498 zenye huduma zilizokamilika ikiwemo huduma
za upasuaji ,tunatoa huduma pia ya mama na mtoto ,lakini pia mkitupa
ridhaa tunampango wa Kuhakikisha kila Kijiji kinakuwa na kituo Cha
afya,pia tunampango wa kuboresha swala la elimu bure kuanzia elimu ya
msingi hadi sekondari katika hili napenda niseme tukipita katika kipindi
hiki ni lazima kila mwananchi atakaezaa mtoto akasome sio ombi bali ni
lazima"alisema Majaliwa
Kwa
upande wa mifugo na uvuvi tumejipanga Kuhakikisha kila mfugaji anafuga
na anapata faida na mkulima analima na kupata faida na ndio maana
tumewatoa maafisa mifugo na maafisa kilimo ofisini na tumewaleta
ukuvijiji kwenu ili wawasaidie.
"Nimesimama
hapa kumuombea Kura Rais wetu pamoja na wabunge na madiwani wapeni Kura
ili tukaweze kutekeleza ilani Hii mpya ya Chama Cha mapinduzi yenye
kurasa 303 na tunauhakika tutaitekeleza zaidi Ile ya awali
2015/2020"alibainisha Majaliwa
Kwa
upande wake mgombea Ubunge wa Jimbo la Monduli Fready Lowasa alisema
kuwa iwapo ata pita Ndani ya siku 100 ataanza na kutatua mgogoro wa muda
mrefu baina ya wakulima na wafugaji uliopo monduli juu pamoja na
changamoto zingine zote zilizopo katika Wilaya ya Monduli.
Kwa
upande wa katibu wa CCM mkoa wa Arusha Mussa Matoroka alisema alisema
kuwa kwa upande wa Jimbo la Monduli Asilimia kubwa ya madiwani wamepita
bila kupigwa .
No comments:
Post a Comment