Na Karama Kenyunko Michuzi TV
OFISI
ya Wakili Mkuu wa Serikali imewaasa mawakili kutoishambulia mahakama
kwenye mitandao ya kijamii na kukumbuka wajibu wao bila kujiingiza
katika mivutano na mihimili ya dola na ikiwa hawajaridhishwa na maamuzi
yotote wakate rufaa ili kupata nafuu nyingine.
Wakili
Mkuu wa Serikali, Gabriel Malata ameyasema hayo leo Agosti 6, 2020
jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya
hukumu ya Mahakama ya Rufaa, iliyotolewa jana, na kuongeza kuwa baada ya
hukumu hiyo, baadhi ya mawakili walipinga maamuzi ya mahakama kwamba
imeshindwa kusimamia katiba.
Amesema
mawakili wanalo jukumu la kusimamia na kuhakikisha sheria zinasimamiwa
huku jamii ikiwa na jukumu la kuzingatia wajibu na haki zao
zinasimamiwa.
Amesema,
kufuatia uamuzi wa mahakama ya Rufaa, watu wameanza kuikejeli mahakama
kwa maneno kama mahakama imeshindwa kusimamia haki za Kikatiba.
"Ninawaomba
mawakili, sisi kama mawakili tuna miiko yetu, hupaswi kuanza
kuishambulia mahakama kwenye Media, kama hujaridhika na maamuzi ya
mahakama unatakiwa kutafuta nafuu nyingine ya ama kukata rufaa au
kutafuta nafuu nyingine yoyote ili kuhakikisha shauri lako linasikilizwa
tena kwa mara nyingine kama unaona unanafasi hiyo." Amesema Malata.
"Ofisi
ya wakili Mkuu wa serikali haitasita kupeleka rufaa katika mahakama za
juu kwa ajili ya kupata nafuu nyingine pindi waonapoona sheria
zinakiukwa.
Ameongeza
kuwa kama jamii inadai sababu za kupelekwa kwa maombi hayo ni
ubambikiziwaji wa kesi, lazima uwepo ushahidi wa kutosha kuthibitisha
madai hayo na kwamba katika kesi hiyo hoja hiyo haijazungumzwa.
"Mahakama
kwa kauli moja ilikubaliana na hoja za serikali kwamba kifungu cha 148
(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai sura ya 20 ya Sheria za
Tanzania hakikinzani na Katiba ya nchi," alisema Malata.
Alisema
jopo la majaji watano waliotoa uamuzi katika kesi hiyo, Jaji Stella
Mugasha, Dk Gerald Ndika, Jacobs Mwambegele, Mwanaisha Kwariko na Ignas
Kitusi, lilibainisha kuwa masharti ya kifungu hicho hayakiuki matakwa ya
Ibara ya 13 (3) na 15(1) (2) ya katiba.
Kwa
mujibu wa hukumu hiyo, maamuzi ya Mahakama Kuu hayakuwa sahihi kwa
sababu katiba ndio inayoruhusu baadhi ya makosa kutokuwa na dhamana.
Akitolea
mfano makosa ya mauaji Wakili Malata amesema, kama ingekuwa watu
wanaofanya matendo ya mauaji wanaachwa kwenye jamii kwa dhamana wale
ndugu wa waliouawa wangefurahi?
Na
ndio maana Bunge liliamua kuweka sheria hii ili makosa makubwa kama
haya ya mauaji na mengine ya uhujumu uchumi, biashara haramu za
binadamu, dawa za kulevya na uhaini kutokuwa na dhamana," alisema Malata
na kuongeza;
"Unapoua
usitarajie mahakama itakupa dhamana kwani ingeruhusiwa kufanya hivyo,
kungekuwa na athari kubwa kwenye jamii ikiwemo usalama wa mtenda kosa
anaweza kuuawa, kupoteza mashahidi na pia itaruhusu kuendelea kwa
vitendo vya mauaji katika jamii."amesema.
Amefafanua
kuwa, kifungu hicho kililenga katika kutekeleza vifungu vya 13(3)
kuhusu wajibu wa mamlaka nyingine za nchi zinazowajibika kulinda usalama
wa raia na mali zao.
Aidha,
amesema katiba kama sheria mama inapaswa kutafsiriwa kwa mapana yake
kwa kuzingatia malengo, maudhui yake katika kulinda haki ya kila mtu na
jamii kwa ujumla na kwamba ikitafsiriwa bila kuhusisha sheria nyingine
ni rahisi kuleta sintofahamu katika jamii.
Amesisitiza
kuwa utaratibu wa kuzuia dhamana ni wa kikatiba kwani wakati ibara ya
15(1) ya katiba inampa mtu haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru,
ibara ya 15 (2) inaruhusu haki na uhuru wa mtu kuingiliwa kwa kufuata
utaratibu uliowekwa na sheria lengo ni kulinda haki na usalama wa jamii.
Mei
18, mwaka huu mahakama Kuu ilitoa uamuzi dhidi ya Maombi hayo na kusema
kwamba Kifungu cha 148 (5) cha sheria ya makosa ya jinai kinakiuka
Katiba.
AG
na DPP walikata rufaa hiyo namba 175/2020 wakipinga uamuzi wa Mahakama
Kuu katika shauri namba 29/2019 lililofunguliwa na Dickson Sanga akitaka
makosa hayo yawe na dhamana kwa sababu kifungu kilichokuwa kinazuia
dhamana, kinakiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wakili
Mkuu wa serikali, Gabrieli Malata akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa
habari jijini Dar es Salaam leo, juu ya uamuzi wa rufaa iliyokatwa na
serikali kupinga hukumu ya mahakama Kuu ya kuruhusu makosa makubwa
kupewa dhamana.
No comments:
Post a Comment