NA MWAMVUA MWINYI, PWANI
MFANYAKAZI wa kazi za ndani mwanaume,Yasin Abdala (35), Kitongoji cha
Kivungwi Kwazoka ,Kata ya Vigwaza Chalinze,Bagamoyo mkoani Pwani
ameuwawa na wananchi wenye hasira kali baada kuwauwa watoto wawili wa
bosi wake ,kwa kuwakatakata mapanga.
Aidha marehemu pia amemjeruhi mama wa watoto hao Sada Salehe (28) kwa
kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili na kukimbizwa kituo cha afya
Mlandizi kwa matibabu zaidi
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi
mkoani Pwani Wankyo Nyigesa alieleza ,tukio hilo lilitokea usiku wa
kuamkia Julai 9 nyumbani kwa Wema Senzie.
Alisema, mtuhumiwa ameuwawa na wananchi waliokwenda kumkamata baada ya
kukimbia alipokuwa amehifadhiwa kwenye ofisi ya Kijiji.
Wankyo ,aliwataja Watoto hao aliowaua ni Abubakary Makolo (6)
mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Kwazoka na mdogo wake
Rehema Makolo (5) mwanafunzi wa shule ya awali Kwazoka.
"Mtuhumiwa baada ya kukamatwa alihifadhiwa ofisini hapo kwa ajili ya
kupelekwa kwenye vyombo vya sheria lakini alivunja mlango na kukimbia
na walipomkamata walimshambulia kwa silaha za jadi na kusababisha kifo
chake," alisema Wankyo.
Wankyo alibainisha, chanzo cha mauaji hayo kinachunguzwa na polisi ila
awali kabla ya tukio hilo mtuhumiwa alikuwa na ugomvi na mama wa
watoto hao.
Miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye kituo cha afya Mlandizi
,kusubiri taratibu za mazishi.
No comments:
Post a Comment