Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias
Kwandikwa (aliyevaa kofia), akitoa maelekezo kwa Meneja wa Wakala
Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Leonard Chimagu,
alipokagua maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege na
sehemu ya maegesho ya ndege.
Meneja wa Ujenzi na Matengenezo
kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Mhandisi Focus Kadeghe, akimwonesha
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa (aliyevaa kofia) tabaka la
barabara ya kuruka na kutua ndege linalojengwa kwa sasa katika upanuzi
wa kiwanja cha ndege cha Dodoma, mkoani humo.
Muonekano wa hatua iliyofikiwa ya
ujenzi wa maegesho ya ndege katika kiwanja cha ndege cha Dodoma. Upanuzi
huo utakamilika mapema mwezi Agosti na kukamilika kwakwe kutaruhusu
ndege kubwa aina ya Airbus zaidi ya tatu kupaki kwa wakati mmoja.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias
Kwandikwa, akitoa maelekezo kwa Meneja wa Ujenzi na Matengenezo kutoka
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Mhandisi Focus Kadeghe, alipokagua
maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege na sehemu ya
maegesho ya ndege katika kiwanja cha ndege cha Dodoma.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias
Kwandikwa, akizungumza na wataalam wa Kampuni ya CHICCO inayotekeleza
mradi wa upanuzi wa kiwanja cha ndege cha Dodoma, wakati Naibu Waziri
huyo alipokagua maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua
ndege na sehemu ya maegesho ya ndege.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias
Kwandikwa (aliyevaa kofia), akimsikiliza Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha
Dodoma, Bi. Bertha Bankwa, akieleza kuhusu maendeleo ya upanuzi wa
kiwanja cha ndege mkoani hapo wakati Naibu Waziri huyo alipokagua
maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kuruka na kutua ndege na sehemu ya
maegesho ya ndege. Kushoto ni Meneja wa Wakala Barabara (TANROADS) Mkoa
wa Dodoma, Mhandisi Leonard Chimagu.
…………………………………………………………………………………
Serikali imewatoa wasiwasi
wafanyabiashara na watumiaji wa usafiri wa anga kwa kuahidi kuanza
ujenzi wa Kiwanja cha Kimataifa cha Ndege cha Msalato jijini Dodoma mara
baada ya taratibu zilizobaki kukamilika.
Akizungumza mjini humo mara baada
ya kukagua maendeleo ya upanuzi wa barabara ya kutua na kuruka ndege na
sehemu ya maegesho ya ndege Naibu Waziri wa Ujenzi, Elias Kwandikwa,
amesema lengo la kutekeleza mradi huo ni kurahisisha usafirishaji kwa
kuruhusu mashirika mengi zaidi kutumia kiwanja hicho.
“Niwahakikishie watanzania kuwa
Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato kitajengwa na kwa wakazi wa
Dodoma ambao wanadai fidia, Serikali itahakikisha wanalipwa kabla ya
kuanza kwa ujenzi huo”, amesema Naibu Waziri Kwandikwa.
Aidha, Naibu Waziri Kwandikwa
ameongeza kuwa kukamilika kwa mradi huo kutaongeza idadi ya ndege
ikiwemo ndege zenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 200 kwa wakati
mmoja.
Naibu Waziri Kwandikwa ameongeza
kuwa Serikali inaendelea kuboresha usafiri wa anga nchini kwa kuendelea
na miradi mikubwa ya uboreshaji wa viwanja vya ndege zaidi ya kumi na
moja nchi nzima vikiwemo vya Lindi, Songea, Shinyanga, Musoma, Songwe
na Mtwara.
Kwa upande wake Meneja wa Wakala
wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Dodoma, Mhandisi Leonard Chimagu, amesema
mradi umefikia zaidi ya asilimia 70 na kuahidi kuendelea kumsimamia
mkandarasi ili kuhakikisha viwango vinazingatiwa.
Mhandisi Chimwangu, ameongeza
kuwa kwa sasa kazi zinazoendelea na ni kuweka tabaka la pili la barabara
ya kuruka na kutua ndege mara baada ya tabaka la kwanza la kushindilia
mawe kukamilika.
Naye Meneja wa Kiwanja cha Ndege
cha Dodoma, Bi Bertha Bankwa, amesema kuwa kukamilika kwa upanuzi wa
sehemu ya maegesho ya ndege utaruhusu ndege zaidi ya nne kupaki kwa
wakati ikiwemo ndege kubwa ya AIRBUS.
Mradi wa upanuzi wa Kiwanja cha
Ndege cha Dodoma, unafanywa na Kampuni ya CHICCO, na unatarajiwa
kukamilika mwezi Agosti mwaka huu na utagharimu kiasi cha shilingi
bilioni 3.5.
No comments:
Post a Comment