HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 22, 2020

WAZIRI MKUU AONGOZA MAOMBI YA PAMOJA KUHUSU KUKABILIANA NA CORONA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Askofu Alex Malasusa wa KKKT Jimbo la Mashariki na Pwani (kushoto), Askofu Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Kuu la Dar es salaam, Yuda Thaddeo Ruwaichi (wa pili kushoto), Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakari Zubeir (wa tatu kushoto) na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (wa nne kushoto) katika maombi ya pamoja kuhusu kukabiliana na tishio la ugonjwa wa homa kali ya mapafu – COVID – 19 kwenye viwanja vya ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Aprili 22, 2020.
Viongozi wa dini wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza katika maombi ya pamoja kuhusu kukabiliana na tishio la ugonjwa wa homa kali ya mapafu – COVID – 19 kwenye viwanja vya ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Aprili 22, 2020.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika maombi ya pamoja kuhusu kukabiliana na tishio la ugonjwa wa homa kali ya mapafu – COVID – 19 kwenye viwanja vya ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, Aprili 22, 2020. Kushoto ni Askofu Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Kuu la Dar es salaam, Yuda Thaddeo Ruwaichi na kulia ni Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad