HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 10, 2019

MAHAFALI YA 30 YA TAASISI YA SANAA NA UTAMADUNI BAGAMOYO (TaSUBa)


Bi. Pili Said Kassimu ambaye ni mmoja wa wahitimu wa ngazi ya Stashahada akipokea cheti kutoka kwa Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Kawawa.

Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Kawawa akitoa hotuba wakati wa mahafali ya 30 ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) ambapo aliwataka wahitimu wakawe raia wema na kuitumia elimu waliyoipata ipasavyo kwa ajili ya manufaa yao na Taifa kwa ujumla. 

Mwenyekiti wa Bodi ya Washauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Bw. George D. Yambesi akitoa neno kwa wahitimu pamoja na kumkaribisha mgeni rasmi kwa ajili ya kutoa hotuba yake.
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Kawawa (katikati) akiwa katika Meza Kuu na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Bagamoyo pamoja na viongozi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni bagamoyo (TaSUBa). 

Wahitimu wakisikiliza hotuba kwa umakini kutoka kwa Mgeni Rasmi ambaye alikua ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Kawawa (hayupo pichani). 

Mhitimu wa ngazi ya Stashahada Bw. David Nashoni akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake mbele ya mgeni rasmi ambaye alikua ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Kawawa.

 




Kikundi cha ngoma kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) kikitoa burudani wakati wa mahafali ya 30 ya Taasisi hiyo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad