HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, November 8, 2019

WADAU UNGANENI KUKABILIANA NA UHARIBIFU WA MISTU NCHINI - RAS TABORA

NA TIGANYA VINCENT
SERIKALI imewataka wadau kuunganisha nguvu zao pamoja katika  kukabiliana na uharibifu wa misitu ya miombo ili kulinda uoto wa asili na kuwa na mistu endelevu kwa ajili ya maendeleo ya ukuaji wa uchumi nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu wakati wa ufunguzi wa warsha ya wadau wa ukanda wa miombo wa Mradi wa Usimamizi shirikishi wa Misitu ya Miombo ya nyanda kame Tanzania.

Alisema pamoja na jitihada zinazofanywa na Serikali na wadau bado kuna kiwango kikubwa cha uharibifu wa mistu ikiwemo ile ya miombo na kusababisha kuwepo na tisho linaloweza kupelekea upotevu wa uoto wa asili.

Makungu alisema uharibifu wa mistu usipothibitwa utasababisha kuwa na gharama kubwa ya kurejesha uoto wa asili uliopotea na wakati mwingine kusababisha kizazi kijacho kushindwa kupata matunda ya mistu iliyoharibiwa.

Alisema Mradi huu wa Uhifadhi wa Misitu ya miombo katika nyanda kame umekuja wakati muafaka ambapo kila wadau wanatakiwa wajiwekee malengo ya pamoja ili kutekeleza Mkakati wa Kuondoa uharibifu wa ardhi na kukabiliana  mabadiliko ya tabianchi.

Naye Mwakilishi Mkazi wa Shirikika la Umoja wa Mataifa la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) nchini Jonathan Sawaya  alisema takwimu zinaonyesha kuwa uharibifu wa mistu hapa nchini ulifikia hekta 469,420 kwa mwaka 2018.

Alisema hali inasababishwa na kuwepo na jitihada kubwa katika kupunguza uharibifu wa mistu na ardhi unaotokana na shughuli za kibinadamu na mabadiliko ya tabia nchi.
Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu (kushoto) akibadilishama mawazo na Mkuu wa Wilaya ya Kaliua Abel Busalama(kulia)  leo wakati wa ufunguzi wa warsha ya wadau wa ukanda wa miombo wa Mradi wa Usimamizi shirikishi wa Misitu ya Miombo ya nyanda kame Tanzania
Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu akifungua leo warsha ya wadau wa ukanda wa miombo wa Mradi wa Usimamizi shirikishi wa Misitu ya Miombo ya nyanda kame Tanzania
Mwakilishi Mkazi wa Shirikika la Umoja wa Mataifa la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) Jonathan Sawaya  akitoa maelezo mafupi kuhusu hali ya uharibifu wa mistu leo wakati wa ufunguzi wa warsha ya wadau wa ukanda wa miombo wa Mradi wa Usimamizi shirikishi wa Misitu ya Miombo ya nyanda kame Tanzania. Picha na Tiganya Vincent
Baadhi ya washiriki wa warsha ya wadau wa ukanda wa miombo wa Mradi wa Usimamizi shirikishi wa Misitu ya Miombo ya nyanda kame Tanzania wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad