HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 26, 2019

TCRA YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA SHULE YA SEKONDARI KIBAHA


Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka hiyo Mhandisi Lawi Odiero (mwenye miwani) akimkabidhi Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibaha Chrisdome Ambilikile hati ya vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) viliyotolewa na TCRA katika hafla kiliyofanyika shuleni hapo Kibaha mkoani Pwani.
Mwakilishi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani ,Katibu Tawala Msaidizi Abdulahman Mdimu akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) vilivyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa Shule ya Sekondari Kibaha iliyofanyika shuleni hapo Kibaha mkoani Pwani.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka hiyo Mhandisi Lawi Odiero akizungumza kuhusiana na vigezo vilivyotumika TCRA kutoa vifaa vya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama)katika Shule ya Sekondari Kibaha.
Mkuu wa Shule ya Sekondari wa Kibaha Chrisdome Ambilikile akizungumza kuhusiana na msaada wa vifaa vya Tehama katika shule hiyo katika hafla ilyofanyika shuleni hapo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Fredrick Ntobi akitoa maelezo kuhusiana na utaratibu wa utoaji wa vifaa vya Tehama kwa Mamlaka hiyo katika shule ya Sekondari.
Mwanafunzi wa Kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Kibaha Samuel Makoye akitoa maelezo kuhusiana na msaada wa vifaa vya Tehama waliopewa katika shule hiyo.
Picha kati ya TCRA,Wanafunzi ,Walimu pamoja na viongozi wa serikali Mkoa wa Pwani 

************************************

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)imesema kuwa itaendelea kusaidia vifaa mbalimbali vya Tekonolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) kwa shule za sekondari zinazofanya vizuri katika matokeo ya mitihani ya kitaifa ili kuweza kuwaanda vijana kuendana na mabadiliko ya sayanasi na teknolojia .

Akizungumza na mara baada ya kukabidhi vifaa mbalimbali vya Tehama Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka, Mkuu wa Kanda ya Mashariki wa Mamlaka hiyo Mhandisi Lawi Odiero amesema kuwa vifaa vya Tehama wanavitoa kwa shule zinazofanya vizuri katika matokeo kidato cha Nne na Tano ambapo ni Kibaha sekondari ni miongoni mwa shule zilizofanya vizuri .

Amesema kuwa vifaa hivyo vitachochea shule hiyo kuendelea kufanya vizuri kwani vitabu mbalimbali vinapatikana katika mitandao ikiwemo na marejemeo mengineyo kwani dunia ndio inakwenda huko.

“Hatutarajii kuona vijana wetu mnatumia vifaa vya Tehama kinyume sheria kwani sheria mtandaoni imeanisha makosa hivyo wanafunzi mtakuwa watu wa kutumia Tehama katika maendeleo ya kufanya vizuri kwa kuendeleza rekodi ya shule ya sekondari Kibaha”amesema Odiero.

Nae Mgeni rasmi Mwakilishi wa Matibu Tawala wa Mkoa Abdulahman Mdimu amesema kuwa wanashukuru kwa msaada waliotoa TCRA na wanafunzi kutunza vifaa hivyo.

Amesema kuwa shule ya Sekondari Kibaha kutokana na kupata kigezo cha kupata vifaa vya Tehama kuongeza juhudi zaidi kwani kuna shule shindani nazo zinahitaji vifaa hivyo.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Kibaha Chrisdome Ambilikile amesema kuwa kutokana na kukua kwa Tehama sasa tunatakiwa kuondokana mfumo wa ufundishaji wa vitabu na daftari ambapo nchi zingine zilishaanza ufundishaji huo.

Amesema kuwa shule inajenga jengo kubwa pamoja na kuweka vyumba vya Tehama ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi waliopo katika shule hiyo na kuongeza kuwa TCRA kuendelea kuingalia shule hiyo kwa jicho linguine kwa kuwaongeza vifaa vvya Tehama.

Mwanafunzi wa Kidoto cha Sita Samuel Makoye amesema kuwa dunia ya sasa imekwenda na mabadiliko mbalimbali ya ya Tehama ambapo wanafunzi lazima tufuate tekonolojia hiyo.

kwani kutumia tofauti na matarajio ni hasara kwani na mtakuwa

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad