HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, November 27, 2019

MLIMBWENDE WA UTALII KUANZA KUTAFUTWA DESEMBA, 2019

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Costantine Kanyasu akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi wa Shindano la kutafuta mlimwende katika utalii (Miss Tourism), katika Hoteli ya Kitalii ya Jaromax iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya Walimbwende wa 2013 na 2014 walioshiriki katika Shindano waliohudhulia semina ya waandano la Miss Utalii.
 Rais wa shindano miss Utalii, Gideon Chipungahelo akizungumza wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wahariri na waandishi wa habari, katika hoteli ya kitalii ya Jaromax iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa Shindano la Mlimbwende wa utalii tukitaka mabadiliko katika urembo ni lazima kufanya mambo mazuri zaidi ya urembo na kuwawezesha washiriki kuwa na maarifa mengi ya masuala ya Utalii.

 Afisa sanaa wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Bona Masenge akizungumza wakati wa semina ya kuwajengea uwezo wahariri na waandishi wa vyomo vya haari jijini Dar es Salaam katika hoteli ya kitalii ya Jaromax iliyopo Mazese jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Sanaa za Maonesho, Wilium Chitanda akizungumza wakati wa Semina ya kuwajengea uwezo wahariri na waandishi wa vyombo vya habari hapa nchini kwaajili ya kuandika habari za Miss Utalii kwa uelewa zaidi. Semina hiyo imefanyika katika Hoteli ya Kitalii ya Jaromax iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam.
 Rais wa shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania(TAFCA), Adrian Nyangamawe akizungumza katika semina ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari katika habari za mlimbwende wa Utalii (Miss Tourism) katika semina iliyofanyika hoteli ya Kitalii ya Jaromax iliyopo Mazese jijini Dar es Salaam.


 Baadhi ya Walimbwende wa 2013 na 2014 walioshiriki katika Shindano waliohudhulia semina ya waandano la Miss Utalii.
Moja ya watoa Mada katika Semina ya kuwajengea uwezo wahariri na waandishi wa habari.

MCHAKATO wa usaili wa kumtafuta mlimbwende wa urembo katika utalii (Miss Tourism) kuanza Desemba, 2019.

Akizungumza na wakati wa semina ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari katika hoteli ya kitalii ya Jaromax iliyopo Manzese jijini Dar es Salaam, Afisa sanaa wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Bona Masenge, amesema kuwa shindano la Mlimbwende katika utalii litaambatana na kutembelea vivutio vilivyopo hapa nchini.

 Bona amesema kuwa BASATA imewaamini waandaaji wa Shindano la Miss utalii kwani kunavigezo mbalimbali ambavyo wamekidhi vya kikanuni, kisheria na kwaajili ya kuandaa shindano hilo.

"Baraza la sanaa Tanzania (BASATA) linahusika na mashindano haya kwa ukaribu ili kuhakikisha waandaaji wa mashindano haya wanakidhi vigezo na kufata taratibu na sheria zilizowekwa na Baraza".
 Amesema Bona

Bona amesema kuwa Shindano la Mlimbwende wa Utalii limeweza kuwapa ajira za kudumu vijana kwa kuinua vipaji vya  vijana wengi na kukuza utalii hapa nchini.

"Mashindano ya mlimbwende wa Utalii yameweza kuinua vipaji kwa washiriki na baadhi wameweza kupata ajira za kudumu na yameweza kukuza utalii kitaifa na kimataifa".

Kwa upande wake Rais wa shindano la miss Utalii, Gideon Chipungahelo amesema kuwa Shindano la Mlimbwende wa utalii tukitaka mabadiliko katika urembo ni lazima kufanya mambo mazuri zaidi ya urembo na kuwawezesha washiriki kuwa na maarifa mengi ya masuala ya Utalii.
Amesema watakaohitaji kushiriki Mahindano hayo wakae mkao wa kula kwani tunata yanayotakiwa ni Mapinduzi Makuwa katika tasnia nchini.

"Miss yourism Tanzania (Mlimbwende wa utalii Tanzania) historia yake kabla na baada ya uhuru shindano la kwanza la kupata mshindi wa dunia katika ulimbwende wa Utalii. 
Amesema Chipunagahelo.


Hata hivyo mchakato huo wa kutafuta Mlimbwende katika utalii utachukua zaidi ya Miezi sita ili kuwapa muda majaji kufanya kazi ya kutafuta Mrembo anayekidhi vigezo vyote na atakayetuwakilisha duniani na kutuletea taji la dunia hapa nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad