HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 18, 2019

BENKI YA CRDB YAKUTANA NA WATANZANIA WANAOISHI NCHINI KOREA

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza na baadhi ya Watanzania waoishi nchini Korea, wakati alipokutana nao kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini humo na kuzungumza nao masuala mbalimbali yanayohusu Benki hiyo. Uongizi wa Benki ya CRDB ulifika ubalozini hapo kwa mualiko wa Balozi Matilda Masuka (kushoto), kwa nia ya kuipongeza Benki hiyo kwa kuwa Benki ya kwanza Afrika Mashariki na Kati, Kupokea kibali cha Umoja wa Mataifa cha Mfuko wa Hali ya Hewa ya Kijani (Green Climate Fund - GCF) itakayoweza kupitisha fedha za utekelezaji wa ufadhili wa kijani nchini Tanzania. Benki ya CRDB ilipata kibali hicho hivi karibuni wakati wa Mkutano wa 24 wa Bodi ya Hali ya Hewa ya Kijani (GCF), huko Songdo, Korea Kusini. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akipeana mkono na Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Balozi Matilda Masuka, baada ya hotuba yake kwa Umoja wa Watanzania waoishi nchini Korea.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay akizungumza katika Mkutano huo.

Baadhi ya Watanzania wanaoishi nchini Korea wakiwa kwenye Mkutano huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad