HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 16, 2019

WASAIDIZI WA AFYA WANUFAIKA NA MRADI WA HPSS


 Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMI, Josephat Kandege akizungumza na wadau wa afya wakati wa kufunga kongamano la Afye lenye ujumbe "The Future of Tanzania Health Supply chain Perfomance Driven by Data and Innovation "  (Tanzania ijayo katika utoaji huduma kwa kuzingatia Takwimu na Uvumbuzi).
Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii

KATIKA kutatua Changamoto ya wahudumu wa ugawaji dawa katika vituo vya Afya nchini mradi wa HPSS tuimarishe Afya umesaidia kusomesha baadhi ya wahudumu wa vituo vya afya nchini.

Kupitia mradi wa kuboresha na kuimarisha Afya nchini wa HPSS wakishirikiana na chuo kikuu cha Afya cha Mtakatifu John kilichopo makao makuu ya nchi Dodoma wamesaidia kuwapa mafunzo wahudumu wa vituo vya afya vilivyopo vijijini katika kutoa elimu ya msingi ya famasia.

Hayo yamesemwa na Mkufunzi wa Chuo cha mtakatifu John, Romuald Mbwasi wakati akizungumza na Michuzi Blog jijini Dar es Salaam leo katika kongamano la wadau wa afya kutoka mikoa mbalimbali ya hapa nchini na nchi za nje.

"Ili kuweza kuondoa tatizo la kuwafanya watu wanaotoa dawa katika vituo vya afya na Zahanati huko vijijini tukaanzisha kozi ya mwaka mmoja ya watoa dawa (Wafamasia) ambao wanapata mafunzo ya kifamasia". Amesema Mbwasi.

Amesema kuwa changamoto kubwa inayowakumba wanaotoa elimu ya wafamasia ni kutokutambuliwa kwa kozi ya mwaka mmoja na utumishi kuajili moja kwa moja serikalini lakini wanaweza kuwaajili kama wahudumu wa saidizi wa afya lakini Serikali inaweza kuwaajili kama wasaidizi wa afya wanaotoa dawa katika vituo vya afya.

Iki kuweza kuziba pengo la wahudumu wa afya wanaweza kuajiliwa kwa kazi maalumu kwa kutoa dawa kuagiza dawa kwa ufasaha zaidi kwa kuwa ndivyo wanavyofundishwa.

Hata hivyo Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMI, Josephat Kandege amewaasa wadau wa afya nchini kote watumie mafunzo waliyofundishwa kwa ufasa hasa wakizingatia takwimu na Uvumbuzi.

 Mkufunzi wa Chuo cha mtakatifu John, Romuald Mbwasi akizungumza na Michuzi Blog jijini Dar es Salaam leo wakati wa kongamano la wadau wa afya kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania pamoja na nchi jirani. Amesema kuwa katika Mradi wa HPSS wameweza kuwezesha maliasili watu wengi ili kuoresha huduma za afya katika vituo vya afya nchini kote.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa -TAMISEMI, Josephat Kandege akizungumza wakati wa kufunga kongamano la wadau wa Afya jijini Dar Es Salaam. 


Baadhi ya wadau wa Afya wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Josephat Kandege jijini Dar es Salaam leo.

Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad