HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, October 17, 2019

PIKIPIKI YA MIGUU MITATU YA MAXIMA Z 3 YA ZINDULIWA JIJINI DAR

WASAMBAZAJI wa pikipiki za miguu mitatu maarufu kama bajaj wa mikoa yote hapa nchini wamejumuika na kampuni ya Sunbeam jijini Dar es Salaam leo kuzindua bajaj mpya aina ya Maxima Z 3 ya ikiwa ni katika mwendelezo wa uboreshaji soko la bajaj sasa.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Meneja wa Mauzo wa kampuni ya Sunbeam, Jestas Kyolike amesema kuwa ameweza kuwaita wasambazaji wa mikoani ili kuja kushiriki pamoja uzinduzi wa bajaj mpya ili waweze kusambaza mikoa mingine.

"Bajaj iliyozinduliwa leo ni bajaj ya kisasa kabisa haijawahi kuwepo hapa Tanzania ni bajaj ambayo ina ingine kubwa na inanafasi kubwa inaweza inaweza ikapita kwenye aina za barabara zetu za Tanzania"
Amesema Kyolike.

Hata hivyo baadhi ya wasambazaji wa bajaj katika Mikoa ya Tanzania wamesema kuwa babaj inaweza kumwinua Mjasiliamali kiuchumi hasa akinunua kwaajili ya biashara ya kubeba abiria katika maeneo yake ya biashara bila kuwa na kikwazo cha jua ama mvua.


 Bajaj aina ya Maxima Z 3 baada ya kuzinduliwa jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa babaj aina ya Maxima Z 3.


 Baadhi ya wasambazaji wa bajaj katika mikoa tofauti hapa nchini wakishuhudia uzinduzi wa babaj aina ya Maxima Z 3 jijini Dar es Salaam.


Meneja wa Mauzo wa kampuni ya Sunbeam, Jestas Kyolike  akizungumza na wafanyabiashara wa bajaj wa mikoa ya Tanzania jijini Dar es Salaam leo. 
 Baadhi ya wasambazaji wa bajaj.
Meneja Mkuu wa Kitengo cha Ufundi wa Kampuni ya Sunbeam, akizungumza ni namna gani wanafanya matengenezo ya bajaj zikiharibika pamoja na kukabiliana na changamoto ya kupatikanaji wa vifaa baada ya bajaj kuharibika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad