HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 1, 2019

RAIS DKT. SHEIN AFANYA UZINDUZI WA MELI YA MAFUTA YA MT.UKOMBOZI II

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasili katika bandari ya Malindi Zanzibar kwa ajili ya Uzinduzi wa Meli ya Mafuta ya MT.Ukombozi II, akiongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Ndg. Mustafa Aboud Jumbe.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Damen Shipyard Gorinchem, Kanda ya Afrika Mr.Ronald Maat, alipowasili katika viwanja vya Bandari ya Malindi Zanzibar kwa ajili ya Uzinduzi wa Meli ya Mafuta ya MT. Ukombozi II, hafla hiyo imefanyika leo 1-10-2019.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Kepteni Azizi na kulia Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Ndg. Mustafa Aboud Jumbe, akiwa katika meli ya mafuta ya MT. Ukombozi II, wakati akitembelea Meli hiyo.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Ndg. Mustafa Aboud Jumbe, wakati akitembelea Meli ya Mafuta ya MT.Ukombozi II, kulia kwa Rais Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Balozi Seif Ali Iddi, Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zuberi Ali Maulid.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, kulia kwa Rais Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Ndg. Mustafa Aboud Jumbe na kushoto kwa Rais Waziri wa Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Mhe.Dr. Sira Ubwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa, wakimsikiliza Msaidizi Nahodha wa Meli ya MT.Ukombozi II Ndg. Ameir Zuberi Kombo , akitowa maelezo wakati wa kutembelea moja meli hiyo baada ya uzinduzi wake uliofanyika leo katika bandari ya Malindi Zanzibar.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akitembelea Meli ya Mafuta ya MT.Ukombozi II, akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Ndg. Mustafa Aboud Jumbe, wakati akitembelea meli hiyo baada ya kuizindua leo katika Bandari ya Malindi Zanzibar.
 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Zuberi Ali Maulid, wakiwa katika chumba cha kuongozea Meli wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Usafirishaji Ndg. Mustafa Aboud Jumbe, akitowa maelezo ya moja ya vifaa vya kuongozea meli wakati wa uzinduzi wa meli hiyo ya MT. Ukombozi II, uliofanyika leo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein,akiwa katika chumba cha kuongozea meli katika ya MT.Ukombozi II, kushoto Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balizi Seif Ali Iddi na Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe.Zuberi Ali Maulid na kulia Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar.Dr. Abdalla Juma Mabodi na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja. Mhe. Hassan Khatib Hassan, wakimsikiliza Msaidizi Nahodha wa Meli ya Mafuta ya MT.Ukombozi II Ndg. Ameir Zuberi Kombo.(Picha na Ikulu)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad