MKURUGENZI
Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, amewaongoza baadhi ya
watendaji wa benki hiyo kugawa chai kwa wateja wao.
Akizungumza
akiwa kwenye tawi la Kariakoo Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Wiki
ya Huduma kwa Wateja, Nsekela alisema ni wiki muhimu kwa wateja wa CRDB.
Alisema
ni wiki ya viongozi wa benki hiyo kutoka matawi yote kuwafuata na
kuwahudumia wateja kwa upendo chini ya kaulimbiu ya 'Ulipo tupo kukupa
Magic'.
"Hii
ni wiki ya huduma kwa wateja duniani kaulimbiu ya dunia ni 'The magic
of service' na sisi benki yetu tunashiriki kwa kuwahudumia wateja wetu.
"Tunawaambia ulipo tupo kukupa Magic. Tumeandaa vitu vingi vizuri naamini wateja wetu watafurahia," alisema Nsekela.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akifungua Shampeni
kuashiria kuanza kwa wiki ya huduma kwa wateja inayoadhimishwa sehemu
mbalimbali duniani, katika hafla iliyofanyika kwenye tawi ya Benki ya
CRDB, Karikoo jijini Dar es salaam.Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akimiminia Shampeni mmoja wa wateja wa Benki hiyo, waliofika kupata huduma kwenye tawi ya Benki ya CRDB, Karikoo jijini Dar es salaam.
No comments:
Post a Comment