HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, September 6, 2019

WATU WENGI ZAIDI KUFAIDIKA NA LUGHA YA KIAFRIKA YA KOMPYUTA


Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.William Ole Nasha akizungumza wakati wa kuzindua wiki ya Lugha ya Kompyuta kwa nchi za Afrika jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa programu ya Lugha ya Komyuta kwa nchini za Afrika hasa Tanzania itasaidia watu wengi kulingana na mahitaji yao ikiwa Tanzania kwa sasa tunakampeni ya kuelekea uchumi wa viwanda tunamahitaji makubwa ya kompyuta hivyo programu hii itasaidia watu wengi zaidi katika nyanja mbalimbali ikiwemo kiuchumi, kilimo, elimu na nyanja mbalimbali zinazohitaji matumizi ta teknolojia hasa ya komyuta.

Amesema kuwa COSTECH pamoja na Ubalozi wa Ireland wawahimize watu kugundua na kutumia teknolojia na kuzielewa programu hizo na sio kutumia pekeyake.
Mkurugenzi mwenza wa  Application ya Girls App, Winnie Msamba akizungumza wakati wa ufunguzi wa Programu ya Lugha ya Kompyuta kwa nchi za Afrika, amesema kuwa watu wengi watafaidi sana kutumia lugha za kompyuta ambazo ni za Kiafrika.


 Baadhi ya wadau malilmbali wa teknolojia wakiwa katika uzinduzi wa Programu ya Lugha ya komyuta ya Afrika jijini Dar es Salaam.
 Mkuirugenzi Mkuu wa tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), DK.Amosi Nungu akizungumza na wadau mbalimbali wa teknolojia jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua programu ya Lugha ya Kompyuta kwa nchi za Afrika amapo amesema kuwa watoto wawe na uwezo wa kujua lugha ya komyuta katika kuelekea uchumi wa Viwanda hapa nchini inahitajika teknolojia ya hali ya juu ili kuleta mawazo mapya ya ukuaji wa uchumi katika nchini za Afrika hasa Tanzania.
 Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Paul Sherlock akizungumza mara baada ya kuzindua Programu ya lugha ya Kompyuta kwa nchi za Afrika jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa UNESCO, Nancy Kaizilege akizungumza umuhimu wa programu ya lugha ya kompyuta kwa nchi za Afrika zitakavyosaidia watu.
Amesema kuwa Lugha ya  Kompyuta inawapa wananchi uelewa wa kuelewa lugha inayotumiwa na waafrika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad