SERIKALI ya Tanzania imeishukuru UNESCO na serikali ya Ireland kwa kufadhili programu ya kuwaendeleza vijana wa kitanzania kidigitali.
Programu hiyo, Africa Code week In Tanzania, imelenga kuwezesha vijana sio tu kujua dunia ya digitali lakini pia kuwa na uwezo wa kubuni na kutengeneza programu mbalimbali zinazogusa teknolojia ya digiti.
Akizungumza wakazi wa uzinduzi wa programu hiyo Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh.William Ole Nasha alisema msaada huo wa serikali ya Ireland ni muhimu kuwawezesha vijana wa Tanzania kupata mafunzo ya tehama ili kusaidia katika mipango ya serikali ya kuwa na uchumi wa kati unaotegemea viwanda.
Naibu Waziri Ole Nasha alisema pamoja na kushukuru Ireland kwa kukubali kudhamini programu hiyo aliwasifu COSTECH na programu yake ya atamizi ambayo inachochea fikira za vijana katika matumizi na maendelelo ya teknolojia hasa upande wa digiti.
Alisema kitendo cha Ireland kusaidia programu hiyo inaamananisha kwamba inasaidia taifa la Tanzania kujenga uwezo wa matumizi ya teknolojia katika dunia ya viwanda na kuwawezesha vijana kutengeneza uwezo wa kujiajiri.
Awali katika uzinduzi huo Balozi wa Ireland nchini, Mh. Paul Sherlock alisema nchi yake imeamua kutoa msaada huo kutokana na kuelewa umuhimu wa kuendeleza vijana ambao ndio wajenzi wa uchumi wa taifa hili kwa miaka mingi ijayo.
Alisema wanaamini kwa kuwa na vijana wengi wenye uwezo wa teknolojia watakuwa wamesaidia kuleta mapinduzi makubwa ya viwanda na pia kutengeneza idadi kubwa ya vijana wenye uwezo mkubwa wa kufanya shughuli zao kisayansi hasa kwenye upande wa uzalishaji.
Alisema kwa miaka ijayo, dunia itategemea zaidi teknolojia ya dijiti kufanya utatuzi mbalimbali wa masuala muhimu yanayohusu uchumi na jamii hivyo vijana zaidi ya milioni 15, wanaotarajiwa kuwapo nchini ifikapo mwaka 2030 watakuwa ni nguvu kubwa kwa nchi ya Tanzania kama watakuwa wanakwenda sambamba na teknolojia ya digiti.
Alisema kwa kuielewa tehama vijana wengi watakuwa wametanzuka na changamoto ya ajira kwani watakuwa wabunifu na wenye uhakika wa kile wanachokitaka katika maisha ya kisasa.
Alisema ni matumaini yake kwamba vijana watatumia programu hiyo vyema kuhakikisha kwamba wanatoka kiushindani.
Awali ilielezwa kuwa mradi huo ulioanza mwaka 2016 kwa mwezi mmoja ujao utafunza walimu 500 ambao watatumika kusambaza maarifa ya code katika mashule mbalimbali, elimu ambayo itatumika kutatua matatizo ya msingi ya jamii.
Naye Mkurugenzi mtendaji wa SAP Ireland, Bw. Liam Ryan amesema kwamba tangu mwaka 2016 ilipoanzishwa Africa Code Week zaidi ya watu 50,000 wamefundishwa na zaidi ya watu milioni 1 wameanza kuifuatilia katika utekelezaji wake.
Alisema wamefurahishwa na mwitikio wa serikali ya Tanzania na anaamini kwamba kwa kuwezesha mafunzo hayo, tehama itafunguliwa kwa mapana yake.
Hata hivyo alisema kwamba wakati umefika wa kuingiza code katika mitaala ili itumike kunoa bongo za vijana ambao ndio dira ya miaka ijayo.
Wakati huo huo Mwalimu Miraji Kunoana kutoka shule ya sekondari ya Twiga alisema ni vyema serikali ikafikiria kuingiza masomo hayo katika mtaala kwa kuwa yatachangamsha akili ya vijana na kunoa bongo zao katika dunia ya digitali.
Alisema mafunzo ambao wameyapata yanawawezesha kufikiria nje ya boksi na kutengeneza chochote wanachotaka katika ubunifu wa teknolojia ikiwamo uumbaji wa vikaragosi na vitu vya kufundishia.
Mwanafunzi aliyefaidika na awamu ya kwanza ya mafunzo hayo Juliet Sewava kutoka Shule ya sekondari ya Tambaza, alishukuru kwa wafadhili wa mradi huo kwani wameweza kutengeneza uwezo wa kiteknolojia na ubunifu.
Anasema wanaweza kwa sasa kutengeneza michezo mbalimbali ikiwemo ya vikaragosi kwa kutumia Code.
Wakati huo huo Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Nancy Kaizilege alisema kwamba mradi huo umelenga kuwezesha vijana kuwa jukwaa la mabadiliko katika matumizi ya tehama kwa manufaa yao na jamii.
Alisema UNESCO YouthMobile imeungana na SAP na wafadhili wengine kuendesha kwa mwaka wa tano Africa Code Week (ACW) kuhakikisha kwamba wanasambaza elimu ya code ili kuwawezesha kukuza zaidi ushiriki wao katika dunia ya teknolojia.
Alisema kuanzia mwaka 2015, zaidi ya watoto milioni 4.1 wameshiriki katika makongamano hayo na kwamba mwaka huu tukio kama la Dar es Salaam katika bara la Afrika wanatarajia kufikia vijana milioni 1.5.
Huku asilimia 43 ya wakazi wake wakiwa na uwezo wa intaneti ukuaji wa teknolojia utabadili maisha ya wananchi wengi katika bara la Afrika na kutengeneza nafasi ya ajira.
Naibu
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh.William Ole Nasha
akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa SAP Ireland, Bw. Liam Ryan
(aliyeipa kamera mgongo) akiwa na Balozi wa Ireland nchini, Mh. Paul
Sherlock (kulia kwa Ryan) pamoja na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na
Habari UNESCO nchini, Nancy Kaizilege (kushoto) mara baada ya kuwasili
katika hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code week
Tanzania iliyofanyika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar
es Salaam.
Kutoka
kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa SAP Ireland, Bw. Liam Ryan,
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Amos
Nungu, mgeni rasmi Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia,
Mh.William Ole Nasha, Balozi wa Ireland nchini, Mh. Paul Sherlock,
Mkurugenzi wa CSR EMEA na Africa Code Week Global Lead wa SAP Ireland,
Bi. Claire Gillissen-Duval pamoja na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na
Habari UNESCO nchini, Bi.Nancy Kaizilege wakiwa meza kuu wakati wa hafla
mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code week Tanzania
iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es
Salaam.
Naibu
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh.William Ole Nasha
akizungumza na wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa hafla mchapalo
ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code week Tanzania iliyofanyika
katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Balozi
wa Ireland nchini, Mh. Paul Sherlock akitoa salamu za serikali ya
Ireland wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code
week Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Bi.Nancy Kaizilege
akitoa salamu za UNESCO YouthMobile wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi
wa Programu ya Africa Code week Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya
Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa SAP Ireland, Bw. Liam Ryan akizungumzia wakati wa hafla
mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code week Tanzania
iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es
Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi), Mramba
Makange akitoa salamu za DTBi wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa
Programu ya Africa Code week Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea
Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Dk. Amos Nungu
akizungumza wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa
Code week Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa
wiki jijini Dar es Salaam.
Mkuu
wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Bi.Nancy Kaizilege
(kulia) na Mkurugenzi wa CSR EMEA na Africa Code Week Global Lead wa SAP
Ireland, Bi. Claire Gillissen-Duval (katikati) wakifurahia jambo wakati
wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code week Tanzania
iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es
Salaam. Kushoto ni Balozi wa Ireland nchini, Mh. Paul Sherlock.
Mwalimu
Miraji Kunoana kutoka shule ya sekondari ya Twiga akitoa ushuhuda wa
Programu ya Africa Code Week ilivyokuwa msaada kwa wanafunzi wa shule
yake wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code
week Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa CSR EMEA na Africa Code
Week Global Lead wa SAP Ireland, Bi. Claire Gillissen-Duval.
Mwanafunzi
aliyefaidika na awamu ya kwanza ya mafunzo ya CODE, Juliet Sewava
kutoka Shule ya sekondari ya Tambaza akitoa shukrani kwa wafadhali na
ujumbe kwa serikali kupitia Wizara ya elimu wakati wa hafla mchapalo ya
uzinduzi wa Programu ya Africa Code week Tanzania iliyofanyika katika
Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya wageni waalikwa na wanafunzi kutoka shule mbalimbali waliohudhuria
hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code week Tanzania
iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es
Salaam.
Mgeni
rasmi Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh.William Ole
Nasha na meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi
walionufaika mafunzo ya Coding kupitia Programu ya Africa Code Week
wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu hiyo ya Africa Code
week Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam
Mgeni
rasmi Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh.William Ole
Nasha na meza kuu katika picha ya pamoja na wageni waalikwa wakati wa
hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu hiyo ya Africa Code week Tanzania
iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es
Salaam
Mgeni
rasmi Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh.William Ole
Nasha na meza kuu katika picha ya pamoja na kamati ya uratibu wakati wa
hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu hiyo ya Africa Code week Tanzania
iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki jijini Dar es
Salaam.
Mkuu
wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Bi.Nancy Kaizilege
(katikati) katika picha ya pamoja na Mwasisi wa Shirika lisilokuwa la
kiserikali la Apps and Girls, Bi. Carolyne Ekyarisiima (kushoto) wakati
wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu hiyo ya Africa Code week
Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mtendaji wa SAP Ireland, Bw. Liam Ryan akizungumza jambo na Naibu
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mh.William Ole Nasha (wa pili
kushoto) wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code
week Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha Kushoto ni Mkurugenzi wa CSR
EMEA na Africa Code Week Global Lead wa SAP Ireland, Bi. Claire
Gillissen-Duval, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia
(COSTECH), Dk. Amos Nungu (katikati), Balozi wa Ireland nchini, Mh. Paul
Sherlock (wa pili kulia).
Balozi
wa Ireland nchini, Mh. Paul Sherlock (kulia)akibadilishana mawazo na
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari UNESCO nchini, Bi.Nancy
Kaizilege (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa CSR EMEA na Africa Code Week
Global Lead wa SAP Ireland, Bi. Claire Gillissen-Duval (katikati)
wakati wa hafla mchapalo ya uzinduzi wa Programu ya Africa Code week
Tanzania iliyofanyika katika Hoteli ya Sea Cliff mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment