HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, September 28, 2019

CGP - PHAUSTINE KASIKE AONGOZA KIKAO KAZI CHA MAAFISA WAANDAMIZI WA JESHI LA MAGEREZA, LEO MKOANI MOROGORO

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike, akisalimiana na Naibu Kamishna wa Magereza, Afwilile Mwakijungu mara baada ya kuwasili kwenye Viwanja vya Nanenane, Mkoani Mororogoro tayari kwa Kikao Maalum cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo. Kikao hicho kimefanyika kwa siku moja leo 28 Septemba, 2019 Mkoani Morogoro.
Kamishna wa Huduma za Urekebishaji na Urekebu, Tusekile Mwaisabila akitoa utambulisho mfupi wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza kabla ya kumkaribisha Kamishna Jenerali wa Magereza kufungua rasmi kikao kazi hicho.
Wajumbe wa Kikao hicho ambao ni Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini maelekezo kutoka kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike (hayupo pichani).
Mkuu wa Magereza Mkoani Lindi, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Josephine Semwenda(kushoto), Mkuu wa Magereza Mkoani Geita, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Edith Mbogo(katikati) na Mkuu wa Magereza Mkoani Pwani, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rehema Ezekiel kwa pamoja wakiteta jambo mara baada ya ufunguzi wa Kikao kazi cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza ambacho kimefanyika kwa siku moja leo 28 Septemba, 2019 Mkoani Morogoro.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, Phaustine Kasike akitoa hotuba ya ufunguzi wa Kikao Maalum cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza leo 28 Septemba, 2019 Mkoani Morogoro.
Meneja wa SACCOS ya Magereza(TPS SACCOS), Kamishna Msaidizi wa Magereza, Abdallah Missanga akitoa ufafanuzi wa huduma mbalimbali zinazotolewa na Chama hicho cha Ushirika cha Jeshi la Magereza mbele ya Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad