WANAFUNZI kutoka shule 100 za mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wamekuwa wakishiriki katika mradi wa tuzo ya uwezo unaoendeshwa na Great Hope Foundation ambapo mapema wikiendi hii kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa walifanya mafunzo ya malengo ya dunia (SDGs) yaliyoambatana na utoaji wa tuzo hizo kwa vijana zaidi ya 100 kutokea shule tofauti.
Mradi huo ulioanza miaka minne iliyopita umelenga kuwawezesha wanafunzi kutambua vipaji vyao na kushiriki katika mafunzo ya ujasiriamali. Aidha mradi huo umetengeneza jukwaa la kumfanya mwanafunzi atambue kwamba elimu ya ujasiriamali ni sehemu ya mafunzo ya kuwezesha ushiriiki wa kuleta maendeleo kwa mujibu wa malengo endelevu ya Umoja wa Mataifa.
Malengo ya maendeleo endelevu ya Umoja wa Mataifa yana vipengele 17 ambavyo ushiriki wa vijana ni muhimu.
Ofisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa nchini (UNIC), Didi Nafisa alisema kwamba mradi huo ni sehemu ya miradi yenye lengo la kutoa mafunzo mbalimbali ikiwamo matumizi ya ubunifu wa kujiongeza katika ujasiriamali.
Alisema katika miradi ya Umoja wa Mataifa, vijana waliofikiwa mpaka sasa ni 60,000 na ambapo wengine wamekuwa wakiendesha miradi ya ufugaji, ujasiriamali, ufyatuaji matofali, na utengenezaji wa vifungashio.
Naye Mratibu wa Kitaifa wa Mradi katika taasisi ya Great Hope, Noelle Mahuvi alisema katika mahojiano kwamba mafunzo hayo ni msaada mkubwa kwa vijana katika kujitambua na kuona kwamba kazi za nje zina mchango mkubwa wa maendeleo.
Alisema wamekuwa wakishirikiana na UNDP katika kuwaelimisha vijana na kuwasaidia katika kusukuma mbele maendeleo kwa kutumia elimu ya ujasiriamali.
Alisema kutokana na mafunzo hayo vijana walioingia chuo kikuu wamekuwa chachu ya wenzao ya kujua manufaa ya ujasiriamali yaani wakiendelea kujifunza darasani na kujifunza nje.
Naye Nancy Faustine mmoja wa wanufaika wa mradi huo kutoka Shule ya sekondari Zanaki amesema kwamba wamefurahishwa na mafunzo kwani yamewezesha wao kurekebisha kantini yao kwa kuipaka rangi na kutengeneza bidhaa za utamaduni na kuziuza.
Alisema mafunzo waliyopewa kupitia tuzo ya uwezo yanatoa mwanga wa kujielewa miongoni mwa vijana na kutambua ushiriki wao katika malengo ya Umoja wa Mataifa ya maendeleo endelevu.
Alisema kupitia mradi huo walipata nafasi ya kuchukuliwa na TANAPA na kutembelea misitu ya Magamba na kutambua ulinzi wa mazingira kama sehemu ya lengo la maendeleo endelevu. Alisema Uwezo Award ni moja ya nyenzo muhimu ya kufundisha kujitambua kwa wahitaji.
Mratibu
wa Kitaifa wa Mradi katika taasisi ya Great Hope, Noelle Mahuvi
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa mafunzo ya
malengo ya dunia (SDGs) yalioendeshwa na Great Hope Foundation kwa
kushirikiana na Umoja wa Mataifa yaliyoambatana na utoaji wa tuzo ya
uwezo kwa vijana zaidi ya 100 kutokea shule tofauti katika hafla
iliyofanyika kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Makongo jijini Dar es
Salaam.
Ofisa
habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa hapa nchini (UNIC),
Didi Nafisa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwa
niaba ya ofisi ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa wakati wa mafunzo ya
malengo ya dunia (SDGs) yalioendeshwa na Great Hope Foundation kwa
kushirikiana na Umoja wa Mataifa yaliyoambatana na utoaji wa tuzo ya
uwezo kwa vijana zaidi ya 100 kutokea shule tofauti katika hafla
iliyofanyika kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Makongo jijini Dar es
Salaam.
Mwanafunzi
wa Shule ya Sekondari Zanaki, Nacy Faustine aliyeshiriki na kuibuka
mshindi wa mradi wa Uwezo Awards unaoendeshwa na Great Hope Foundation
nchini akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ushiriki wake na jinsi
alivyonufaika na mradi huo wakati wa mafunzo ya malengo ya dunia (SDGs)
yalioendeshwa na Great Hope Foundation kwa kushirikiana na Umoja wa
Mataifa yaliyoambatana na utoaji wa tuzo ya uwezo kwa vijana zaidi ya
100 kutokea shule tofauti katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa
shule ya sekondari Makongo jijini Dar es Salaam.
Bbaadhi
ya wanafunzi walioshiriki kutengeneza miradi kupitia mafunzo ya taasisi
ya Great Hope wakitoa shuhuda za miradi waliyobuni wakati wa mafunzo ya
malengo ya dunia (SDGs) yalioendeshwa na Great Hope Foundation kwa
kushirikiana na Umoja wa Mataifa yaliyoambatana na utoaji wa tuzo ya
uwezo kwa vijana zaidi ya 100 kutokea shule tofauti katika hafla
iliyofanyika kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Makongo jijini Dar es
Salaam.
Ofisa
habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa(UNIC), Didi Nafisa
akiendesha mafunzo ya malengo ya dunia (SDGs) kwa washiriki 100 kutoka
shule za mkoa wa Dar es Salaam na Pwani yaliyoambatana na utoaji wa tuzo
ya uwezo kwa vijana hao katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa
shule ya sekondari Makongo jijini Dar es Salaam.
Ofisa
habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa(UNIC), Didi Nafisa
akielezea utekelezaji wa malengo 17 ya dunia (SDGs) wakati wa mafunzo
ya SDGs yalioendeshwa na Great Hope Foundation kwa kushirikiana na Umoja
wa Mataifa yaliyoambatana na utoaji wa tuzo ya uwezo kwa vijana zaidi
ya 100 kutokea shule tofauti katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa
shule ya sekondari Makongo jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya wanafunzi kutoka shule mbalimbali wakiwa wameshika baadhi ya malengo
ya dunia SDGs wakati wa mafunzo ya SDGs yalioendeshwa na Great Hope
Foundation kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa yaliyoambatana na utoaji
wa tuzo ya uwezo kwa vijana zaidi ya 100 kutokea shule tofauti katika
hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Makongo jijini
Dar es Salaam.
Baadhi
ya walimu kutoka shule za Dar es Salaam na Pwani walioshiriki mafunzo
ya malengo ya dunia (SDGs) yalioendeshwa na Great Hope Foundation kwa
kushirikiana na Umoja wa Mataifa yaliyoambatana na utoaji wa tuzo ya
uwezo kwa vijana zaidi ya 100 kutokea shule tofauti katika hafla
iliyofanyika kwenye ukumbi wa shule ya sekondari Makongo jijini Dar es
Salaam.
Baadhi
ya wanafunzi wa shule za Dar es Salaam na Pwani walioshiriki mafunzo ya
SDGs yalioendeshwa na Great Hope Foundation kwa kushirikiana na Umoja
wa Mataifa yaliyoambatana na utoaji wa tuzo ya uwezo kwa vijana zaidi ya
100 kutokea shule tofauti katika hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa
shule ya sekondari Makongo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment