HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, July 30, 2019

POLISI YAPOKEA MSAADA WA MAGARI MAWILI NA PIKIPIKI KUMI

Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Simon Sirro akikata utepe pamoja na maafisa wawakilishi wa Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA) Bwana Rene Becker (kulia) na Bwana Harald Gessner (kushoto) kuashiria makabidhiano ya msaada wa magari mawili na pikipiki kumi kwa Polisi kutoka Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA). Hafla ya kupokea msaada huo imefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Polisi. 
Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Simon Sirro akipokea pikipiki miongoni mwa msaada wa magari mawili na pikipiki kumi kutoka kwa maafisa wawakilishi wa Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA) Bwana Rene Becker (kushoto) na Bwana Harald Gessner. Hafla ya kupokea msaada huo imefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Polisi.
Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Simon Sirro akiwasha gari miongoni mwa msaada wa magari mawili na pikipiki kumi kutoka kwa maafisa wawakilishi wa Shirika la Upelelezi la Ujerumani (BKA) Bwana Rene Becker (kulia) na Bwana Harald Gessner. Hafla ya kupokea msaada huo imefanyika leo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam. Picha na Jeshi la Polisi. 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad