HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, May 5, 2019

SPIKA NDUGAI AONGOZA HARAMBEE UJENZI WA VYOO SHULE YA MSINGI KARUME MKOANI DODOMA

 Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai akizungumza na wananchi wa Kibaigwa wakati wa harambee kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya wanafunzi wa Shule ya Msingi Karume iliyopo Kibaigwa Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma. Katika harambee hiyo mifuko 763 ya Saruji ilipatikana, fedha kiasi cha Sh. 2, 645, 900 viliziweza kuchangwa ambapo taslimu ilikuwa ni 1,225, 900 na Ahadi 1, 420, 000/=
 Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa,. Job Ndugai (wa pili kushoto) akiongozana  na viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa wakati alipowasili na kwenda kukagua ujenzi wa vyoo vya wanafunzi wa Shule ya Msingi Karume iliyopo Kibaigwa Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
 Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (wa tatu kulia) akimsikiliza Afisa elimu Kata ya Kibaigwa, Ndg. Adilla Muna wakati akikagua ujenzi wa vyoo vyaF wanafunzi wa Shule ya Msingi Karume iliyopo Kibaigwa Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.
 Wananchi Mbali mbali wa Kibaigwa wakimsikiliza Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (hayupo kwenye picha) wakati wa harambee kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya wanafunzi wa Shule ya Msingi Karume iliyopo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma. Katika harambee hiyo mifuko 763 ya Saruji ilipatikana, fedha kiasi cha Sh. 2, 645, 900 viliziweza kuchangwa ambapo taslimu ilikuwa ni 1,225, 900 na Ahadi 1, 420, 000/=

Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (wa pili kulia)akipokea zawadi ya mfuko wa saruji kutoka kwa Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Bima la Taifa, Ndg. Elisante Maleko (wa pili kushoto) tukio lililofanyika leo katika Shule ya Msingi Karume iliyopo Kibaigwa Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma. Shirika la Bima la Taifa lilitoa mifuko 530 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyoo vya wanafunzi wa Shule ya Msingi Karume.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad