HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 13, 2019

Jumuiya ya Wazazi CCM yaita kikao cha dharura

Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imekutana na kwa dharura katika kikao cha Kamati ya Utekelezaji chini ya Mwenyekiti wake, Dk. Edmund Mndolwa.

Kikao hicho kimefanyika leo Ofisi Ndogo za CCM Lumumba, jijini Dar es Salaa, ambapo kitajadili masuala mbalimbali ya chama.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Siasa na Oganizesheni ya Jumuiya ya Wazazi, Chollaje Mohamed, alisema kuwa kikao hicho kipo chini ya uenyekiti wa Dk. Mndolwa.

"Bado tunaendelea na kikao, ni kako cha dharura cha kamati ya utekelezaji ya Taifa. Pindi kitakapokamilika tutatoa taarifa kamili," alisema Chollaje
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Edmund Mndolwa akizungumza kwenye Kikao cha dharura cha kamati ya utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi Taifa kilichofanyika leo katika ukumbi wa ofisi Ndogo ya  CCM Lumumba jijini Dar es Salam.
Baadhi ya wajumbe wakiwa kwenye kikao hicho

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad