HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 15, 2019

WASOMI NCHINI WAASWA KUTUMIA ELIMU YAO VIZURI KUIKOMBOA JAMII

Na Ahmed Mahmoud, Arusha

Wahitimu nchini wameaswa kutumia elimu yao vizuri katika kuwa chachu ya kuwakomboa wengine katika changamoto mbalimbali zinazowakabili ndani ya Jamii.

Hayo yalisemwa Jana na Mwenyekiti wa umoja wa wanawake ccm mkoa wa Arusha, Yasmin Bachu wakati akizungumza katika mahafali ya 20 ya wanafunzi 154 wa kidato cha sita katika shule ya sekondari Enaboishu iliyopo mjini hapa.

Alisema kuwa, wanapaswa kutumia elimu hiyo waliyoipata kuwa watatuzi wa changamoto mbalimbali katika jamii kwani wao Ndio wanaotegemewa kuleta mabadiliko chanya.

Aidha aliwataka wanafunzi hao pia kuhakikisha wanatoa elimu na kupinga vitendo viovu vya madawa ya kulevya kwa vijana sambamba na kupiga vita unyanyasaji wa kijinsia ambao ndio umeshamiri katika jamii nyingi kutokana na mila na desturi zilizopo.

"nawaombeni jamani mkawe mfano wa kuigwa na muwe mabalozi wazuri wa kabadilisha Jamii Kwa kutoa elimu Kwa vijana wenzenu juu ya vitendo mbalimbali viovu, ili kupitia nyie tuweze kuona mabadiliko makubwa. "alisema Bachu.

Kwa upande wa Mkuu wa shule hiyo, Godwin John alisema kuwa, shule hiyo imekuwa ikiwandaa wanafunzi kufanya vizuri ikiwemo kutoa motisha kwa wanafunzi wanaofanya vizuri pamoja na walimu ili kuongeza kiwango cha ufaulu zaidi shuleni hapo.

Alisema kuwa, shule hiyo imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vioo vya vyumba vya madarasa, ukosefu wa madarasa, ulipaji ada wa kusuasa hivyo kuwataka wazazi pamoja na walezi kuhakikisha wanawekeza zaidi kwa watoto wao kwani huo ndio urithi pekee unaotakiwa kutolewa kwa watoto.

Naye Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Titi mzava aliwataka wanafunzi hao kutobweteka na elimu hiyo waliyoipata badala yake wakawe mfano bora wa kuigwa katika kuitangaza shule hiyo.

Aidha aliwataka wanafunzi hao pindi wanaporejea mtaani wakawe chachu ya mabadiliko kwa vijana wenzao kupitia elimu hiyo waliyoipata.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad