NA MWAMVUA MWINYI, PWANI
MAHAKAMA ya hakimu mkazi Mkuranga, mkoani Pwani, imemtia hatiani, Sifa
Livigha kwa kumpa adhabu ya kifungo cha nje na kutotenda kosa katika
kipindi cha miezi sita (conditional discharge) baada ya kufuja fedha
kiasi cha sh. milioni mbili.
Aidha mshitakiwa ameamriwa kulipa fedha kiasi cha sh. milioni 2
,alizokuwa anashitakiwa kuzifuja kinyume na kifungu cha 28 cha sheria
ya kuzuiana kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 .
Hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Mkuranga, Janet Kinyage amemtia
hatiani ,Livigha kwa mujibu wa kifungu cha 38(1) cha sheria ya kanuni
ya adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Anasema Livigha alifikishwa mahakamani hapo tarehe 03/05/2018 kwa kosa
moja la kufanya ubadhilifu na ufujaji wa fedha hizo kinyume na kifungu
cha 28 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka
2007.
Mtuhumiwa alikuwa mwenyekiti wa kitongoji cha Mivule, kijiji cha
Mwanambaya wilayani Mkuranga na alifikishwa mahakamani baada ya mwaka
2104 kupokea fedha za ushuru wa kijiji na kuzifuja bila kuziwasilisha
ofisi ya kijiji.
Nae kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Pwani, Suzan Raymond alitoa wito kwa
wananchi wote popote walipo kuacha kujihusisha na vitendo vya rushwa,
badala yake watumie nafasi walizo nazo katika mapambano dhidi ya
rushwa.
Vile vile aliwaasa kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa njia ya
simu ya bure namba 113 (maarufu kwa jina la Longa Nasi) au kwa
kufika ofisini pindi wanapobaini uwepo wa vitendo vya rushwa.
No comments:
Post a Comment