HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, April 15, 2019

BENKI YA CRDB, UBA WAUNGA MKONO JUHUDI ZA SERIKALI UTEKELEZAJI WA MRADI WA UMEME WA MAJI WA RUFIJI

BENKI ya CRDB kwa kushirikiana na Benki ya UBA (Tanzania) zimedhamini utekelezaji wa mradi wa umeme wa maji wa Rufiji (Rufiji Hydro Power Project) unaotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), ikiwa ni mkakati wakusaidia juhudi za Serikali kukamilisha mradi huo.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema kuwa Benki ya CRDB ikiwa benki ya kizalendo imeamua kuungana na jitihada za Serikali kufanikisha miradi mbalimbali, na sasa wametilia mkazo katika mradi huo muhimu unaolenga kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme nchini.  

Kwa upande wa Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Mwinyimvua Hamisi alisema, dhamana hizo zilizokabidhiwa ni muhimu sana katika kuhakikisha kwamba utekelzaaji wa mradi wa bwawa la kufua umeme wa maji wa mto Rufiji unaanza bila kuchelewa na kuhakikisha kwamba ratiba iliyokubaliwa baina ya serikali na mkandarasi itatekelezwa kwa mujibu wa mkataba.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Shaaban alisema “Jambo hili la uwekaji wa dhamana ni muhimu sana kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu kwani ni mradi wenye gharama kubwa kiasi cha shilingi za kitanzania trilioni 6.6 kwa hivyo ni mradi unaogharimu fedha nyingi katika historia ya nchi yetu katika miaka ya hivi karibuni.” Alisema Bi. Amina.

Kwa upande wake Naibu Gavana wa BoT, Dkt. Benard Kibese alisema, kazi kubwa ya BoT katika utekelezaji wa mradi ni kuweka mazingira mazuri ili kuhakikisha ushiriki wa taasisi za fedha za hapa nchini unakuwa mkubwa.

Mwisho kabisa Mkuurgenzi Mtendaji wa TANESCO Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka aliishukuru serikali ya awamu ya tano chini wa uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwezesha hatua hiyo kufikiwa kwani mradi huo bila pesa kulipwa mkandarasi hawezi kufanya kazi yake ipasavyo. Dkt. Mwinuka alisema hatua ya leo inawezesha pesa kulipwa kwa mkandarasi pale zitakapohitajika au pale ambapo mkandarasi anastahili kulipwa kwa hivyo kuanzia sasa utekelezaji wa mradi huu hautakuwa na kikwazo chochote katika ulipaji wa pesa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Ally Laay akiwa na Mkurugenzi Mtedanji wa benki hiyo, Abdulmajid Nsekela (wa tatu kushoto) wakimkabidhi hati za dhamana Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO,  Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka (wa nne kulia), katika hafla fupi, iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam. walioshuhudia ni Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Mwinyimvua H. Hamisi, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi.Amina Shaaban, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Dkt. Bernard Kibese, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Bw. Charles E. Kichere na Balozi wa Misri hapa nchini Mhe.Mohammed Gabel Abulwafa. Wakandarasi wanaotekeleza mradi huo wanatoka nchini Misri.
Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. Mwinyimvua Hamisi akizungumzia umuhimu wa utekelezaji wa mradi wa bwawa la kufua umeme wa maji wa mto Rufiji, unaotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), katika hafla hiyo, iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam.
Balozi wa Misri nchini Tanzania, Mohamed Gabel Abulwafa akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Amina Shaaban akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Bernard Kibese akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO,  Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka akizungumza katika hafla hiyo, iliyofanyika leo kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam.











No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad