HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, March 14, 2019

WASHINDI 15 WAPATIKANA PROMOSHENI YA TIA KITU PATA VITUUZ NA DSTV

Na Khadija Seif, Globu ya Jamii
KAMPUNI ya Multichoice nchini  kupitia king'amuzi cha Dstv imechezesha droo ya tatu ya promosheni ya  tia vitu upate vituuzi jijini Dar es salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Mkuu wa kitengo cha thamani kwa wateja Hilda Nakajumo wakati wa kutangaza washindi hao 15 waliopatikana katika kila vifurushi kama Compart plus, family,  premier pamoja na kifurushi cha bomba amesema ni wakati wa wateja kunufainika na na kuendelea kuuwasha kupitia king'amuzi hicho.

"Leo tumefanikiwa kupata washindi 15 kutoka mikoa mbalimbali kama vile Arusha, Kagera, Manyara pamoja na Dar es salaam na inaonyesha wazi kuwa  king'amuzi cha Dstv kinaendelea kutoa huduma nzuri na gharama nafuu, alisema Nakajumo"

Aidha amesema washindi hao wamezawadiwa malipo ya miezi miwili bure ili kuendelea kufaidika na vipindi mbalimbali kupitia King'amuzi cha Dstv.

Hata hivyo kwa upande wake Afisa Mwandamizi wa bodi ya michezo ya kubahatisha  Humud Abdulhussein amesema ni wakati wa wateja wa Dstv kulipia ving'amuzi vyao kwa wakati ili kupata ofa hiyo .

"Hakuna mtu ambaye anapangwa kwenye droo na pia inachezeshwa kwa haki bila ujanja wowote ambapo vigezo na masharti vinazingatiwa ipasavyo ," alisema  Abdulhussein.

Na Mshindi wa kifurushi cha Compart  mkazi wa jijini Mwanza Musa Juma mwenye umri wa miaka 24 amewapongeza Dstv kwa promosheni hiyo ya tia vitu pata vituuzi.

"Sikutegemea kama ningeweza kushinda katika droo hii ya tatu mara nyingi nasikia tu wenzangu wakishinda nikajaribu bahati yangu na nikaamua kulipia kwa wakati king'amuzi changu hatimae nimeibuka mshindi," alisema Juma

Pia amewapa ujasiri wateja wengine kulipa kwa wakati ili waweze kuingia kwenye droo hiyo na kushinda kabisa.
Mkuu wa kitengo cha thamani kwa wateja Kampuni ya Multichoice kupitia king'amuzi cha Dstv Hilda Nakajumo(katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza washindi 15 waliopatikana katika droo ya tatu ya promosheni ya tia kitu pata vituuzi akiwa pamoja na  Afisa Mwandamizi wa bodi ya michezo ya kubahatisha Humud Abdulhussein(kulia) .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad