Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu
Hassan anaondoka nchini leo kuelekea Kampala, Uganda kushiriki kwenye
Mkutano wa mwaka 2019 wa ‘Africa Now Summit’unaotarajiwa kufanyika tarehe12 na 13 Machi.Mhe. Makamu wa Rais anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Mkutano
huo utafunguliwa na Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni ambaye
ndiye mwenyeji wa mkutano huu. Mkutano utakuwa na mada mbalimbali
ikiwemo ya Uongozi unaohitajika kuchochea mabadiliko ya Kijamii na
Uchumi Afrika, mada hii itatolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Viongozi
wengine watakaotoa mada ni Rais wa Misri ambaye pia ni Mwenyekiti wa
Umoja wa Afrika (UA) Mhe. Abdel Fattah el Sisi; Rais wa Afrika Kusini
Mhe. Cyril Ramaphosa; Makamu wa Rais wa Kenya Mhe. William Ruto; na
Waziri Mkuu wa Ethiopia Mhe. Ahmed Abiy. Mada zote hizi zitajikita
kwenye kuonesha chachu ya Uongozi katika kuleta maendeleo endelevu
barani Afrika.
Mkutano
utamalizika tarehe 13 Machi 2019 utaanza na hotuba kutoka kwa Rais wa
Somalia Mhe. Mohamed Abdullahi na baadae kufungwa rasmi na mwenyeji wake
Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni.
Makamu wa Rais ataambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro.
Imetolewa na:
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es salaam
11/03/2019
No comments:
Post a Comment