Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega amefanikiwa kumaliza changamoto katika sekta ya elimu iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa Wilaya ya mkuranga kwa kipindi kirefu hasa kwa watoto walifaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kushindwa kuripoti kutokana na ukosefu wa madarasa.
NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Abdallah Ulega amefanikiwa kumaliza changamoto katika sekta ya elimu iliyokuwa ikiwakabili wananchi wa Wilaya ya mkuranga kwa kipindi kirefu hasa kwa watoto walifaulu na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kushindwa kuripoti kutokana na ukosefu wa madarasa.
Akizungumza na wananchi wa Mkuranga
wakati alipokuwa akikagua shule 3 za sekondari zilizojengwa kwa nguvu ya
wananchi kwa kushirikiana na serikali katika kata za Njia nne, Mwandege na kata
ya Tambani, Ulega amesema kuwa serikali ya awamu ya Tano imetoa zaidi ya
milioni 200 ili kumalizia shule hizo ili wanafunzi waweze kuanza masomo mara
moja.
Amesema kuwa awali palikuwa na
changamoto kubwa na hivyo kupelekea wanafunzi waliomaliza darasa la saba mwaka
jana kukosa shule ya sekondari huku wakiwa na ufaulu wa hali ya juu, amezitaja
shule zilizopata msaada huo kutoka kwa serikali ni pamoja na Mwandege, Njia nne
na shule iliyopewa jina lake la Abdala
Ulega sekondari.
“Wazazi wenzangu mnatakiwa
kuwasimamia watoto wetu waweze kuwa katika maadili mema ili kuwa mfano wa
kuigwa nchini kwani itafikia hatua mimi nitastaafu hivyo lazima tuwe na wasomi
wengi katika wilaya yetu ya mkuranga na hiyo yote elimu ndio msingi mkubwa.”
amesema Ulega.
Aidha Ulega ametoa mifuko 40 ya
saruji, zaidi ya milioni tatu kwa kila shule ili kuhakikisha mwezi wa
tatu wanafunzi hao wanaanza shule mara moja ili kutowaweka wanafunzi hao katika
hatari nya kupata vishawishi vitakavyokatisha ndoto zao hasa mimba.
Kwa upande wake Afisa elimu wa
sekondari wa Wilaya hiyo Benjamini Majoya amempongeza Naibu waziri kwa jinsi anavyopambania elimu katika wilaya
hiyo ili iweze kukua na hiyo ni kwa namna anavyojitolea katika kuhakikisha miundombinu
inakuwa rafiki kwa wanafunzi.
Akitoa taarifa za elimu wilaya humo
Afisa elimu huyo amesema kuwa mara baada
ya Serikali kutoa kiasi cha pesa hicho kupitia kwa Naibu waziri Ulega shule
hizo zitakamilika haraka na wanafunzi 1071 ambao bado hawajaanza shule
wataanza mara moja na kumaliza changamoto kwa wanafunzi hao.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya
Mkuranga Firbeto Sanga amesema kuwa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais
John Pombe Magufuli imekuwa ni serikali ya utekelezaji kwa vitendo kuliko
maneno hasa katika kuhakikisha sekta muhimu zinaangaliwa kwa makini Zaidi.
Aidha amempongeza Naibu waziri wa
Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega kwa jinsi anavyopambania kuipaisha wilaya hiyo
katika masuala ya maendeleo mbalimbali hasa miundombinu ya barabara, shule,
hospitali mengine mengi.
Naibu Waziri Mifugo na Vuvi (MB) wa Mkurangara , Abdallah Ulega akizungumza na wananchi mara baada ya kukagua ujenzi wa madarasa katika kata Njianne, Mwandege na Tambani, leo Wilayani Mkuranga.(Picha zote na Emmanuel Massaka,MMG)
Naibu Waziri Mifugo na Vuvi (MB) wa Mkurangara, Abdallah Ulega akikagua madarasa yaliyojengwa na wananchi pamoja na Serikali huku ikitegemewa Machi mwaka huu yataanza kutumika kwa wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza, leo Wilayani Mkuranga.
Afisa Elimu wa Sekondari wilaya ya Mkuranga,Benjamini Majoya akiwahakikishia wazazi na walezi wa wilezi shule hizo zitafunguliawa mwezi wa tatu mwaka huu,(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
Muonekano wa Madarasa ya shule hizo ambazo ni; Shule ya Sekondari iliyopewa jina la mbunge huyo Abdallah Ulega, Tambani na Njia nne.
No comments:
Post a Comment